Sunday, May 4, 2014



 20140502_111547
Na Baraka Mpenja, Dar es Salaam
KOCHA mpya wa Taifa Stars, Mart Nooij anatarajia kuiongoza timu hiyo kwa mara ya kwanza katika mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya timu ya taifa ya Malawi kwenye  uwanja wa Sokoine jijini Mbeya leo jioni.
Hiki ni kipimo kizuri cha Nooij kujua makali ya kikosi chake ambacho kiliweka kambi tangu aprili 27 mwaka huu,  mjini Tukuyu kujiandaa na mchezo huo ikiwa ni harakati za kujiweka sawa kabla ya kuanza kusaka tiketi ya kushirki kombe la mataifa ya Afrika mwakani nchini Morocco.
Stars yenye mchanganyiko wa wachezaji wakongwe na wale waliopatikana katika mpango wa maboresho ya Taifa stars wana jukumu kubwa la kuwaaminisha watanzania kuwa watafuzu AFCON mwakani.
Mechi iliyopita ya kirafiki, Aprili 26 mwaka huu walichapwa mabao 3-0 na akina Didier Kavumbagu, Amisi Tambwe na Yusuf Ndikumana wa Burundi.
Huo ulikuwa mchezo maalum wa  kuadhimisha miaka 50 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibara ambapo timu ya taifa ya Burundi iliizidi kwa kila kitu Taifa stars iliyosheheni wachezaji wengi kutoka kikosi cha maboresho.
Kwa mara ya kwanza katika historia ya soka, uwanja wa Sokoine utatumika kwa mechi ya Taifa stars.
Wapenzi wengi wa soka mkoani Mbeya wamefurahishwa na maamuzi ya TFF kuipeleka mechi hii mkoani humo.
Hii imetokana na jitihada kubwa ya viongozi wa chama cha soka mkoani Mbeya, MREFA na wamiliki wa uwanja wa Sokoine, CCM katika kuuboresha uwanja  na kuwa na hadhi ya mechi ta Taifa stars dhidi ya Malawi.
 20140502_095807
Uongozi wa MREFA umewaomba wapenzi wa soka jijini Mbeya kujitokeza kwa wingi kuishangilia Taifa stars leo hii ili kuwaaminisha watanzania kuwa Mbeya ni mji uliojaa wapenda soka.
Kwa miaka mingi Stars imekuwa ikicheza zaidi Shk. Amri Abeid, Arusha, CCM Kirumba, Mwanza, na shamba la bibi au Taifa, jijini Dar es saala, lakini safari hii imekuwa zamu ya sokoine.
Mwenyekiti wa MREFA, Elias Mwanja ameuambia mtandao huu kuwa maandalizi yote yamekamilika na hali ya hewa ni nzuri, hivyo kinachosubiriwa kwa sasa ni muda kufika.
“Nawaombe mashabi wa soka jijini Mbeya kujitokeza kwa wingi ili kuishangali timu yao ya Taifa”.
“Hii ni fursa adimu mno, wasiwaangushe watanzania wenzao. Kwapamoja twendeni tukaishangilie timu yetu kwa moyo mmoja”. Alisema Mwanjala.
Kiingilio katika mechi hiyo ya kimataifa ni shilingi elfu tano tu (Tsh 5,000/=.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video