Saturday, May 10, 2014



 http://kandanda.galacha.com/wp-content/uploads/2014/04/aisha-manula.png
Na  Baraka Mpenja, Dar es salaam
KWA niaba ya wachezaji wenzake, mlinda mlango namba moja na nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania chini ya miaka 20, Ngorongoro Heroes, Aishi Manula amekaririwa na mtandao huu akiwaomba wapenzi wa soka kujitokeza kwa wingi kuwaunga mkono katika Mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20.
Haya ni maneno ya vijana wetu wanaojiandaa kuwakabili Nigeria  kesho jumapili kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam majira ya saa 10:00 jioni.
Ngongoro wamefikia raundi ya pili baada ya kuwatoa Kenya kwa penati 4-3 kufuatia kutoka suluhu ya bila kufungana  katika mechi zote mbili.
Kocha wa Ngorongoro, John Simkoko anakabiliana na Fly Eagles wenye historia nzuri katika soka la vijana barani Afrika.
Hii itakuwa mechi muhimu kwa Tanzania, hivyo jambo jema kwa mashabiki ni kujitokeza kuwashangilia vijana hao kama walivyoomba.
Mechi dhidi ya Kenya haikuwa na watu wengi sana, lakini mechi dhidi ya Nigeria mashabiki wana nafasi kubwa ya kuwapa motisha wachezaji kwa kujitokeza kwa wingi uwanjani kwasababu wana nafas kubwa ya kuisaidia timu.
Mashabiki ni mchezaji wa 12, TFF wamefanya kazi yao, John Simkoko kafanya kazi yake, wachezaji wamejiandaa kwa nafasi zao na wataingia kushindana kesho, watu pekee waliosalia kutimiza wajibu wao ni mashabiki wa soka.
Watanzia twendeni tukaishangilie timu yetu kwasababu ikipata mafanikio itakuwa faida na heshima kwa Tanzania.
Kutokana na ubora wa Nigeria, kuna ulazima mkubwa wa Ngongoro kupata magoli angalau matatu nyumbani ili kujiweka mazingira mazuri ya kufuzu katika mechi ya marudiano.
Vijana wetu watambue kuwa kuna utofauti mkubwa wa Nigeria na Kenya, hivyo watatakiwa kuwa na nidhamu kubwa uwanjani.
Kwa vile Simkoko yupo nyumbani, bila shaka atataka  kumilikia mpira na kushambulia zaidi ili kupata magoli mengi, lakini wakati vijana wake wakicheza hivyo, ni lazima kuzingatia ubora wa Nigeria kwasababu wanaweza kubadili matokeo wakati wowote.
Hakuna haja ya kuwaogopa Nigeria, kikubwa wachezaji wetu wajiamini na kuona wao ni bora zaidi.
Walinde lango lao, wacheze mpira na kushambulia. Kama watafanya kazi hizi tatu tunatarajia kupata matokeo. Lakini cha msingi zaidi kila nafasi watakayoipata waitendee haki.
Nidhamu ya mpira itahitaji sana kwasababu Nigeria ni watu makini na wanajua kutumia makosa ya wapinzani, na hii si tu kwa timu za vijana, hata timu ya wakubwa wanaweza kucheza sana mpira.
 Fainali hizo za 19 za Afrika zitafanyika mwakani nchini Senegal zikishirikisha timu saba zitakazofuzu kwenye mechi za mchujo, na Senegal wanaoingia moja kwa moja kutokana na kuwa wenyeji.
  
Viingilio katika mechi hiyo ni sh. 2,000 kwa sehemu zote wakati upande wa VIP itakuwa sh. 5,000. Tiketi zitauzwa uwanjani siku ya mechi katika magari maalumu.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video