Saturday, May 10, 2014



 _DSC0648
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
BEKI  na nahodha wa zamani wa Yanga sc, Ally Mayay Tembele ameshauri viongozi wa timu za Tanzania kuachana na mfumo wa kutoa mikataba mifupi kwa makocha wao kwasababu zipo katika harakati za kutafuta maendeleo.
Mayay ameueleza mtandao huu kuwa kwa bahati mbaya klabu zetu hazina utamaduni na falsafa zao za kucheza mpira, hivyo kila mwalimu anakuja na mfumo wake.
Akitumia mfano wa Simba sc, Mayay alisema ndani ya kipindi kifupi wamekuwa na makocha wanne na kupata athari kubwa katika michuano ya ligi kuu.
“Kumbuka kwa mfululizo, Simba wamebadili makocha. Aliondoka Milovan Circovic, akaja Patric Liewig, baadaye wakamleta Abdallah Kibadeni, na mwanzoni mwa mzunguko wa pili wa msimu uliopita akaletwa Dravko Lofarusic”.
“Kwa asimilia kubwa kufanya vibaya kwa Simba kumechangiwa na athari kubwa ya mabadiliko ya makocha”.
“Kila kocha ana falsafa yake. Na kwa bahati nzuri Simba wana wachezaji wengi vijana ambao ni rahisi kumeza falsafa za makocha makocha wao”.
“Vijana kama Ramadhan Singano, Ndemla, Mkude, Chanongo wanafundishika kirahisi kutokana na umri wao”.
_DSC0659Kocha mkuu wa Simba sc, Dravko Logarusic (wa kwanza kushoto)


“Milovan ana falsafa yake ambayo huitumia. Kuna aina ya mpira anataka wachezaji wake wacheze, na wachezaji wanaanza kuzoea mfumo huo”.
“Ghafla analetwa mfaransa Liewig, naye anaanza upya na mfumo wake, wachezaji wanaanza kuuzoea, mara analetwa Kibadeni mwenye mfumo wake”.
“Wachezaji wakiwa katika harakati za kuuzoea mfumo wa kibadeni, ghafla analetwa Mcroatia Loga. Naye analeta mfumo wake”.
“Haya yanatokea kwasababu klabu haina falsafa yake. Huwezi kujua upi ni utamaduni wa uchezaji wa Yanga ua Simba”.
“Timu zinabadilika badilika kutokana na aina ya walimu wanaoletwa”. Alifafanua Mayay.
Aidha, aliongeza kuwa kwa wenzetu kila klabu ina falsafa yake, huku akitolea mfano wa soka la Barcelona.
 Mayay alisema hata aje mwalimu kutoka wapi, ni ngumu kubadili mfumo wa soka la Barcelona na kinachotakiwa kwa  makocha ni kuingiza baadhi ya mbinu za kiufundi lakini si kubadili mfumo mzima wa uchezaji.
“Angalia Guardiola anavyohangaika kuibadili Bayern yenye utamaduni wake. Inakuwa ngumu kwasababu wamejengwa katika falsafa fulani na utamaduni wa soka la Ujerumani”.
SAM_2259Aliyekuwa kocha wa Yanga sc, Hans Van der Pluijm ( wa kwanza kulia)
Akizungumzia kuondoka kwa kocha wa Yanga baada ya kuiongoza klabu kwa miezi mitano tu, Mayay alisema si jambo geni kwasababu amemaliza mkataba wake, lakini akasema litaleta athari kwa klabu.
“Yanga wamekaa na kocha wao miezi mitanotu  baada ya kumaliza mkataba wake wa miezi sita. Pluijm alianza kuijenga Yanga katika misingi fulani”.
“Ilikuwa inacheza mpira tofauti na ilivyokuwa kwa Ernie Brandts, sasa wakati wachezaji wakiiva katika mfumo wa Pluijm wanajikuta wakianza upya na kocha mpya msimu ujao”.
“Kama atakuja na mfumo mpya, maana yake Yanga wataanza upya kiuchezaji”.
“Nawashauri wawe na tabia ya kuwapa makocha mikataba mirefu, angalau kuanzia miaka miwili.”
Mei 8 mwaka huu, kocha  mkuu wa Young Africans, Mholanzi, Hans Van der Pluijm aliondoka Yanga baada ya kupata kazi mpya nchini Saudi Arabia na tayari alishaaga na kuondoka zake.
Pluijm aliyejiunga na Yanga mapema januari mwaka huu umepata shavu hilo katika klabu ya Al Shoalah FC inayoshiriki ligi kuu soka nchini Saudi Arabia.
Yanga chini ya Pluijm ilimaliza katika nafasi ya pili, huku Azam fc chini ya kocha Mcameroon, Joseph Marius Omog wakibeba taji lao la kwanza tangu wapande ligi kuu msimu wa 2008/2009. 

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video