Na Baraka Mbolembole
Golikipa wa Shaaban Kado tayari ameanza mazoezi baada
ya kuondoa plasta ngumu ( P.O.P) ambayo alifungwa tangu mwezi machi baada ya kuvunjika
sehemu ya mkono wake.
Akizungumza na mtandao huu kipa huyo aliyemaliza mkataba wake na timuya
Coastal Union yaTanga, amesema tayari ameanza kujifua wakati akitafakari wapi
pa kwenda kucheza msimu ujao.
Amekanusha kila uvumi unaomuhusisha yeye na klabu za
Azam FC na Simba SC, huku akisema kuwa ana malengo tayari hivyo ukifika wakati atafikia
maamuzi.
“ Kwasasa naendelea vizuri, nimeanza mazoezi binafsi.”
Anasema mlinda mlango huyo wa Tanzania ambaye aliwahi kushinda tuzo ya kipa
bora wa ligi kuu katika msimu wa mwaka 2008/09 akiwa na kikosi cha Mtibwa
Sugar. Kado yupo huru tangu April 24, lakini bado hajawa tayari kuweka wazi ni wapi
atacheza kuanzia msimu ujao.
“ Mimi sijasikia chochote kuhusu kutakiwa na timu hizo
( Simba , Azam) hivyo siwezi kuzungumza lolote. Nina malengo yangu hivyo wakati
ukifika kila kitu kitakuwa wazi” anasema, Kado ambaye ameitwa mara kadhaa katika
timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars na hadi anaumia alikuwa katika kikosi hicho
ambacho kilicheza na timu ya Nambia, mapema mwezi machi mwaka huu.
Stars itacheza na Zimbabwe siku ya jumapili hii katika
uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mchezo
wa kwanza kati ya miwili ya mtoano kuwania kufuzu kwa hatua ya makundi ya kufuzu
kwa fainali za Mataifa ya Afrika, 2015, Nchini, Morocco, Kado kwa upande wake
anasema ni wakati wa kuisapoti timu hiyo na ana imani kuwa kila mchezaji tayari
anajua majukumu yake kuelekea katika mchezo huo.
“ Ni, wajibu kuiombea timu yetu ipate matokeo mazuri
katika uwanja wa nyumbani. Kila mchezaji atakuwa anafahamu majukumu yake na kwanini
yupo pale ( Stars). Muhimu ni kupata ushindi wa kutosha. Brazil iliyotajwa na Scorali
inaweza kutwaa ubingwa bila kuwa na wachezaji wazoefu “”
Wakati michuano ya kombe la dunia ikitaraji kuanza
kutimua vumbi lake, Juni, mwaka huu katika nchi ya Brazil, Kado kama ilivyo kwa
Watanzania wengi naye tayari ana timu ambayo ataisapoti katika michuano hiyo ya
21.
“ Mimi ni shabiki wa Brazil, timu imara na ni timu
ya michuano. Naipenda tu, Brazil namna wanavyocheza na vipaji walivyonavyo.
Sina shaka na uteuzi wa kocha Scorali ( Luiz) katika uteuzi wake, naamini amefanya
machaguo sahihi ya wachezaji, na tusisahau kuwa Brazil ndiyo ‘ wafalme wa kandanda
duniani’, ni timu yenye vipaji vingi hivyo unapoona kocha anawaacha wachezaji kama,
Ricardo Kaka’ na Robinho basi jua tayari amekuwa na mbadala wao”
0 comments:
Post a Comment