Milionea: Messi amekubali kusaini mkataba mpya Barcelona ambao utamfanya awe mwanasoka anayelipwa zaidi ya wote duniani.
MSHAMBULIAJI
Lionel Messi atakuwa akilipwa Pauni Milioni 16.3 kwa mwaka katika
mkataba mpya aliokubali kusaini na klabu yake, Barcelona jambo linalomfanya Muargentina huyo kuwa mwanasoka anayelipwa zaidi duniani.
Baba
wa mchezaji huyo Jorge alikutana na viongozi wa klabu hiyo Javier Faus
na Antoni Rossich wiki iliyopita na kufikia makubaliano ya mkataba wa
saba ndani ya miaka 11 ya mshindi huyo wa Ballon d’Or nne Barcelona.
Messi atafikisha miaka 27 June na mkataba mpya unatarajiwa kuweka Camp Nou hadi mwaka 2018.
Kwa
mshahara huo mpya, Messi anampiku hasimu wake, Cristiano Ronaldo wa
Real Madrid ambaye analipwa Pauni Milioni 15 kwa mwaka.
0 comments:
Post a Comment