MSHAMBULIAJI
wa zamani wa Manchester United, Luis Saha ameunga mkono Ryan Giggs kupewa
nafasi ya kuwa kocha wa kudumu Old Trafford.
Giggs
aliteuliwa kuwa kocha wa muda wa Man United baada ya David Moyes kutimuliwa
mwezi uliopita akiwa amefanya kazi miezi 10 tu katika mkataba wake wa miaka 6.
Mechi
ya kwanza ya United chini ya mkongwe huyo raia wa Welsh ilishinda mabao 4-0
dhidi ya Nowrich City kwenye dimba la Old Trafford jumamosi iliyopita na
atakuwa kwenye kibarua chake kwa mechi tatu zilizosalia.
Kocha
Mholanzi, Louis van Gaal amekubali kazi ya kuifundisha Man United, huku Giggs akitarajiwa
kuwa sehemu ya benchi lake la ufundi, lakini Saha ametaka mchezaji mwenzake
huyo wa zamani kupewa nafasi hiyo.
“Namjua
Ryan atakosa nafasi na nadhani anastahili kupewa ukocha wa kudumu”. Saha
ameuambia mtandao wa Sky Sports News.
“Ni
fursa kubwa kwake. Kiukweli ana sifa zote, ana mvuto na ni mstahimilivu. Hakuna
wasiwasi juu ya hilo”.
“Amekosa
uzoefu tu, lakini unapocheza Manchester United kwa zaidi ya miaka 20 unajua
namna ya kufanya kazi”.
“Labda
siko sahihi, lakini nadhani inahuzunisha, nadhani angepewa mwezi mwingine
kutulia na kuonesha kuwa ni chaguo sahihi. Mechi nne hazitoshi”.
0 comments:
Post a Comment