Friday, May 16, 2014



daaa0fe1055eb07463e4e6f1cd61cf79
Na Baraka Mbolembole
Nani atathubutu kumwita tena Robinho De Souza ni ' Pele Mpya'? Wakati, Pele ' mfalme wa kandanda duniani ' alianza kucheza katika ligi kuu ya Brazil akiwa na miaka 16 katika klabu ya Santos, mechi yake ya kwanza tu akafunga goli. Mwaka mmoja baadaye akiwa kinda wa miaka 17 akaitwa katika timu ya Taifa ya Brazil, ' Selecao- Wateule' ambako alifanya ' maajabu' makubwa ambayo hayajafikiwa na mchezaji yeyote Yule hadi sasa.
Licha ya kuwa na umri mdogo, na ikiwa mara yake ya kwanza kucheza katika fainali za kombe la dunia, Pele aliisaidia, Brazil kutwaa ubingwa huo katika fainali zilizofanyika nchini, Sweden, 1958, huku akiibuka mfungaji bora wa pili akiwa amefunga magoli sita.
Alishinda mara tatu ubingwa wa dunia, na hadi anastaafu soka akiwa na miaka 28, Pele alifanikiwa kufunga jumla ya magoli 1281 katika michezo 1363 za kimashindano akiwa na klabu ya Santos na timu ya Taifa.... Katika msimu mmoja, Pele aliwahi kufunga magoli 127 , mwaka 1959 akiwa na Santos katika michuano yote, alifunga magoli 110, mwaka 1961, na alifunga magoli 101, mwaka 1961. Mfalme huyo wa kandanda duniani alifunga magoli matatu matatu katika mchezo mmoja ' hat-trick' mara 92, na aliifungia Brazil jumla ya magoli  97. 
robinho
Moja kati ya matukio ya kukumbwa daima kwenye fainali za kombe la dunia, 2002, ilikuwa ni kitendo cha winga, Denilson kukokota mpira mpaka kwenye kona ya uwanja na kuzunguka nao akiwapiga chenga za maudhi mabeki, huku akikabwa na nusu ya wachezaji wa timu ya Uturuki. Selecao, walikuwa mbele kwa goli 1-0 katika mechi ya nusu fainali huku zikiwa zimebaki dakika chache mpira umalize, watangazaji wa mpira na mashabiki walipagawa kwa furaha, wakisifu kipaji cha winga huyo wa zamani, Denilson kama kielelezo halisi cha soka la Brazil.
Katika hali ambayo ni vigumu kuamini, mwaka mmoja baadaye aliibuka kijana mahiri mwenye kipaji kikubwa cha kupiga chenga za maudhi, Robinho de Souza. Alikuwa kinda wa miaka 18 wakati alipoisaidia klabu ya Santos kufika fainali ya klabu bingwa Amerika Kusini na kufungwa na Boca Junior. Wakati, Pele alitumia muda wake mwingi kucheza soka katika klabu ya Santos, Robinho alitangaza kipaji chake na haraka timu kubwa barani Ulaya zilianza kumfukuzia. Alijunga na Real Madrid, mwaka 2005 akiwa ameifungia Santos magoli 73 katika kipindi cha miaka mine.
 hi-res-105210687_crop_north
TAMAA YA PESA AU AMEANGUSHWA NA KUKIMBIA CHANGAMOTO?.
Akiwa na miaka tisa kwasasa barani Ulaya, Robinho ameshindwa kufanana na Pele, kitabia, kiuwezo, na kimafanikio, alionekana kuwa mbioni kufikisha walau michezo 100 ya kimataifa akiwa na Selecao, lakini ameishia kuiwakilisha nchi yake mara 92 na kufunga magoli 27. Ni mafanikio makubwa kuiwakilisha nchi yenye vipaji vingi vya uhakika kama Brazil. Lakini kama mchezaji ambaye alifananishwa na Pele kiuchezaji ni aibu kutumia kipindi kirefu barani Ulaya na kushindwa kufika walau katika orodha ya wachezaji watano bora katika tuzo ya mwanasoka bora wa dunia.
Katika misimu yake miwili ya mwanzo, Madrid, Robinho aliweza kuwa mchezaji tishio, alionekana kuwa na kipaji kikubwa ndani ya uwanja. Akiwa amepewa jezi namba 10 iliyokuwa ikivaliwa na gwiji, Luis Figo, nyota huyo wa Brazil alifanikiwa kufunga magoli 14 katika michezo 37, msimu wake wapili alifanikiwa kuisadia Real kutwaa ubingwawa La liga huku akiibuka mfungaji bora watatu nyuma ya Raul Gonzalez na aliyekuwa mfungaji bora, Ruud Van Nistelrooy, huku pia akionesha kipaji kikubwa katika upigaji wa pasi za mwisho, jambo ambalo lilimfanya kuwa nyuma ya kiungo Gutti katika vinara wa pasi za magoli katika La Liga.
Baada ya kuonyesha kiwango cha hali ya juu katika michuano ya Copa Amerika, mwaka 2007, Robinho alionekana kama mchezaji bora duniani nyuma ya Mbrazil mwenzake, Ricardo Kaka' lakini miaka miwili baadaye alipigana kulazimisha uhamisho wa kuondoka, Madrid kwa madai ya kuchukizwa na kitendo cha rais wa klabu hiyo kumfanya chambo ili amnase, Cristiano Ronaldo kutoka, Manchester United.
Robinho aliiwakilisha, Brazil kwa mara ya kwanza mwaka 2003 akiwa na miaka 19 katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Mexico, mara ya mwisho aliitwa na kocha wa sasa, Luiz Fillipe Scorali katika michezo miwili ya kujipima nguvu dhidi ya Honduras na Chile. Scorali alimuita nyota huyo kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2011. Wapenzi wengi wa soka wanasema kuwa kitendo cha nyota huyo kuhama, Madrid na kukataa ofa ya kwenda Manchester United, Chelsea na kuichagua, Manchester City kilisukumwa na mambo ya kifedha zaidi ya kimpira.
United ilikuwa ikitamba barani Ulaya na kwa stahili yake ya uchezaji, Robinho angeweza kutamba na kung'ara zaidi barani Ulaya, ila mshahara wa pauni 300,000 kwa wiki ulihitimisha matarajio ya ' Pele Mpya'. Alitua, City kwa ada ya rekodi, England, pauni milioni 32 na alifanikiwa kuonyesha makali yake mwanzo mwa msimu wa 2008/09 lakini taratibu alianza kushuka kiwango chake cha umakini, uchezaji na kujituma. Aliamua kurudi, Santos kwa mkopo ili kujiweka sawa na fainali za kombe la dunia mwaka 2010. Baadaye alihamia, AC Milan na hadi sasa bado yupo katika kikosi hicho ambacho alikisadia kushinda ubingwa wa Seria A, msimu wa 2010/11.Amefungia Milan magoli 27 tu katika michezo 107 ndani ya misimu minne.Aliifungia Real Madrid magoli 25 katika michezo 101 ndani ya misimu mitatu.
Baada ya kucheza michezo zaidi ya 360, kufunga magoli 199, kushinda mataji matatu makubwa barani Ulaya katika kipindi cha miaka tisa, nani atathubutu tena kumuita Robinho De Souza ‘ Pele Mpya’? Kwasasa klabu ya Flamengo inamuwinda nyota huyo ili kumrudisha nyumbani. Je, Robinho anaweza kuibuka tena? Ameachwa na kocha Scorali katika kikosi cha Brazil ambacho kitashiriki katika kombe la dunia mapema mwezi ujao katika ardhi ya nyumbani kwao. Ana miaka 3o kwasasa hivyo kurejea ni jambo linalowezekana kwa kuwa yeye ni Mbrazil, na amekosa nafasi kutokana na sababu hizo za yeye kuwa Mbrazil, nchi yenye vipaji kila kona.
0714 08 43 08

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video