BEKI
mkongwe wa Manchester United, Rio Ferdinand anaamini Louis van Gaal ni mtu
sahihi kukabidhiwa majukumu ya ukocha mkuu klabuni hapo.
Kutangazwa
kwa Mholanzi huyo kama mirthi wa David Moyes kulistishwa jana alhamisi ili
kumuacha huru wakati huu akiiandaa timu ya taifa ya Uholanzi kucheza mechi ya
kirafiki dhidi ya Ecuador.
Van
Gaal amewahi kuongeza klabu kubwa za dunia, hivyo beki huyo wa kati ambaye hatakuwepo Old
Trafford msimu ujao baada ya kutangaza kuondoka majira ya kiangazi mwaka huu
amesema kocha huyo anaweza kuleta mafanikio katika michuano ya ligi kuu.
“Anaonekana
mtu imara sana na muelekezaji. Ana uelewa na ufahamu mkubwa kwa kila anachotaka
kufanya. Unatakiwa kuwa hivyo katika klabu kama Man United,” Ferdinand
aliwaambia waandishi wa habari.
“Katika
klabu alizopita-Ajax, Bayern Munich, Barcelona- anaonekana kufanya mambo kwa falsafa
yake na nadhani atafanya hivyo akiwa na Man United.”
Van
Gaal ataelekeza nguvu kubwa ligi kuu ya England katika msimu wake wa kwanza
kwasababu Ma United walishika nafasi ya 7 na kushindwa kufuzu michuano ya
Ulaya, na Ferdinand anasema mazingira hayo yatawafanya warudi kwenye mbio za
ubingwa”.
Ferdinand
kwasasa anafirikiria wapi kwa kwenda kucheza. Beki huyo mwenye miaka 35
anahusishwa kwenda nchini Uturiki, lakini Asernal na Hull City zinaonesha nia
ya kumtaka.
0 comments:
Post a Comment