Friday, May 16, 2014



 World Cup in Qatar a mistake, admits Blatter
RAIS wa FIFA, Sepp Blatter amekiri kuwa walifanya makosa kuwapa Qatar uenyeji wa fainali za kombe la dunia za mwaka 2022.
Qatar waliwashinda wapinzani wao Marekani, Korea kusini, Japan na Australia, lakini maamuzi ya FIFA kuwapa nafasi ya kuhodhi michuano hiyo yalikoselewa vikali tangu yalipothibitishwa desemba mwaka 2010.
Sababu kubwa ya watu wengi kupinga Qatar kuwa mwenyeji wa kombe la dunia ni kwasababu ya joto kali majira ya kiangazi ambapo kombe hilo hufanyika.
Hata hivyo FIFA walipotangaza maamuzi yao, mwaka mmoja baada iliibuka kashfa ya rushwa ambapo ilielezwa kuwa Qatar waliwahonga maofisa wa FIFA na kuwepa uenyeji wa fainali hizo za mwaka 2022.
Aidha, shiriki la kutetea haki za binadamu la kimataifa limewataka FIFA kuingilia kati kwani kuna taarifa za kunyanyaswa kwa wafanyakazi wanaojenga viwanja katika taifa hilo la Gulf.
Siku za nyuma, Blatter alikuwa anatetea uamuzi wa FIFA kuwa ulikuwa sahihi kuwapa uenyeji Qatar, lakini kwasasa amekiri kuwa ilikuwa makosa.
“Kiukweli yalikuwa makosa (kuwapa uenyeji wa kombe la Dunia Qatar)”. Blatter amewaambia RTS.
“Lakini wote tunajua kuwa makosa yanatokea katika maisha”.
“Ripoti za idara ya ufundi kutoka Qatar zilieleza kuwa majira ya kiangazi kuna joto kali sana. Hata hivyo haikuzuia kamati kuwapa uenyeji wa fainali za kombe la dunia, tena kwa kura nyingi”.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video