Tuesday, May 6, 2014



 _DSC0696
Na Baraka Mpenja, Dar es saalaa
Tel: 0712461976
MWANASHERIA Damas  Ndumbaro amepewa jukumu la kuongoza kamati ya uchaguzi wa Simba sc kwa lengo la kupata warithi wa viongozi wasasa wanaoongozwa na mwenyekiti, Ismail Aden Rage.
Kamati ya uchaguzi imeanza kazi hiyo baada ya serikali kukabidhi katiba iliyofanyiwa marekebisho kwa uongozi wa Simba sc.
Uchaguzi wa Simba ulitakiwa kufanyika wiki iliyopita, lakini mapungufu katika vipengele kadhaa katika katiba yao yalikwamisha .
Lakini jana katibu mkuu wa Simba sc, Ezekiel Kamwaga alitangaza kuwa tayari serikali imemaliza zoezi lake na kukabidhi katiba.
Kwa misingi hiyo, Kamati ya uchaguzi haina cha kupoteza zaidi ya kuanzisha rasmi mchakato mzima wa kupata viongozi wapya wa klabu.
Tangu Rage aingie madarakani miaka miwili iliyopita kumekuwepo na changamoto nyingi na mivutano isiyoisha.
Si rahisi kujua kama Rage alikuwa mbaya katika uongozi wake kwasababu inasemekana kuna watu wachache walikuwa hawampendi ndani ya uongozi na kupandikiza chuki kwa wanachama ili aonekane hafai.
Majaribio kadhaa ya kutaka kumpindua Rage yameshuhudiwa bila mafanikio.
Katiba ya Simba imekuwa ikimlinda kwa wakati wote, hivyo wale wanaojaribu kumpindua kugonga mwamba.
Unakumbuka sakata la aliyekuwa kaimu mwenyekiti wa Simba, Joseph Itang`are `Mzee Kinessi` na baadhi ya wajumbe wa kamati ya utendaji.
Kinessi alitangaza kumsimamisha mwenyekiti Rage, lakini mwanaume huyo aliyekuwepo nje ya nchi alirudi na kuita kikao chao kama kikao cha harusi na yeye atabaki kuwa mwenyekiti.
Hata TFF walitangaza kumtambua na akaendelea na majukumu yake klabuni.
Pia wanachama wa baadhi ya matawi walishakutana mara kadhaa kutaka kumpindua Rage, lakini waliishia kuzodolewa na mkuu wao huyo.
Rage aliweza kuyafanya hayo kwa misingi ya katiba ya Simba waliyoiandika wanachama wenyewe.
Wakati Rage anaingia madarakani, alikuja na mipango mizuri ili kuiweka Simba klabu ya kisasa.
Aliahidi kujenga uwanja mzuri wa klabu, lakini ndoto zake ziliyeyuka baada ya kutokea migogoro.
Inasemekana kuna watu walimsaliti Rage na kufanya kazi ya kueneza sumu kwa wanachama. Ni ngumu kubaini hayo kwasababu mambo mengine yapo chini ya kapeti.
Inawezekana Rage ana mapungufu yake kama ilivyo kwa binadamu yeyote, lakini namna ya kujua mapungufu haya lazima uwe na hoja iliyojengwa kwa umakini mkubwa.
Rage kaifanyia mengi klabu yake, lakini kwasababu watu wengi wanaamini hafai, basi yanaokena mabaya zaidi kuliko mazuri.
Hakuna haja ya kuumiza kuzungumza juu ya Rage ambaye tayari ameshatangaza kutogombea tena katika uchaguzi ujao.
Wanachama wa Simba umefika muda wa kumtoa madarakani Rage ambaye wengi wenu mnaona hafai kwa mujibu wa katiba.
 http://api.ning.com/files/hiOw4xekqhksYSIhoxeTTtxodHT6pCSfY1vYjpjIa*mqvthtiybXpfvpesMEvV6qdY1*8mV5pVAVMc4F4W0o7*hK7toNkjwn/rage1.JPG
Klabu zinazoendeshwa na wanachama kama ilivyo kwa Simba na Yanga, wa mwaka au mkutano mkuu wa uchaguzi ndio kila kitu.
Sasa Rage anaondoka, kazi kubwa ni kumpata mrithi wake wa kuendeleza mazuri yake na kufuta mabaya yake.
Kama kwa muda mrefu mlikuwa mnataka mpiganaji Rage aondoke Simba, umefika wakati wa yeye kukaa pembeni.
Kumbukeni soka limebadilika nchini Tanzania. Kwa mipango mibovu, Simba imemaliza nafasi ya nne msimu uliopita.
Msimu wa mwaka juzi mlimaliza nafasi ya tatu. Kwa misimu miwili mnakosa michuano ya kimataifa.
Najua mnaikumbuka Simba yenu ya 2003 na ile ya akina Okwi misimu miwili iliyopita.
Simba ilikuwa hatari sana, lakini siku za karibuni imekuwa na matokeo mabaya na sasa kuanza kuonekana timu ya kawaida.
Zamani timu kukutana na Simba ilikuwa shughuli pevu, lakini msimu uliopita watu walikuwa wanajipigia kirahisi.
Ni kweli Simba mpo kwenye mpito kwasasa. Lakini wakati wa mabadiliko umeshawadia.
Kwa muda mrefu wachezaji wa Simba wamekuwa wakilalamika chini kwa chini kuwa uongozi wa Rage umeshindwa kuboresha mishahara yao.
Pia ucheleweshaji wa mishahara na posho imekuwa tatizo. Hata siku wakienda Zanzibar kujianda na mechi ya Yanga, wachezaji kwa saa kadhaa waligoma kuingia kwene boti kwa kushinikiza kulipwa pesa zao.
Zacharia Hans Poppe aliokoa jahazi na tuliona mpira wenu mkubwa uwanja wa Taifa na Yanga ambapo wanajangwani walihangaika kuchomo o bao na kulazimisha sare ya 1-1.
Pia kumekuwepo na mabadiliko ya mfufulizo katika benchi la ufundi, hivyo kuleta athari kubwa.
Simba imekuwa ikienda mbele na kocha huyu, lakini ghafla analetwa mwingine na falsaya mpya na kuanza upya.
Bahati nzuri kocha wa sasa, Dvrako Logarusic ameaminiwa na ataandeleza pale alipofikia mwaka huu na tayari ameshakabidhi ripoti yake na mapendekezo ya usajili.
 http://1.bp.blogspot.com/-W8puIqNsc-4/UepgSoMoAnI/AAAAAAAAv1E/6w8SXUhEBk0/s640/16.JPG
Tayari kamati ya usajili chini ya  mwenyekiti wake, Zacharia Hans Poppe ipo kuijadili ripoti hiyo kuanzia jana jumatatu na itamaliza kesho jumatano.
Wakati kamati ya usajili ikiwa katika majadiliano, nayo kamati ya uchaguzi chini ya mwenyekiti wake Damas Ndumbaro inakutana leo hii kupanga mchakato wa uchaguzi na tarehe ya kufanyika.
Hatua hizi mbili ni kubwa sana. Usajili na uchaguzi.
Simba inategemewa kuleta sura mpya katika kikosi na uongozi.
Watu wapya na mambo mapya. Kikubwa umakini uanzie kwenye mambo haya mawili.
Watu wa usajili wafanye kazi nzuri na kutekeleza mipango ya kocha wao ili kuimarisha kikosi chao.
Kama watasajili vizuri, Simba itarudi katika kasi yake msimu ujao.
Pili, uchaguzi ni jambo lingine nyeti sana. Hapa wanachama imebaki kwenu.
Kama kwa muda mrefu mnamlaumu Rage, sasa imefika wakati wa kuchagua viongozi wapya.
Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya viongozi na timu kufanya vizuri uwanjani.
Viongozi wakiwajibika vizuri kulinda maslahi ya makocha na wachezaji, mpira lazima uonekane.
Kuweni makini na watu wenye nia ya kuomba uongozi. Chunguzeni na pimeni sera zao.
Kuna watu wanaitwa wachumia matumbo. Hawa wanaingia katika klabu kusaka tonge.
Kwa viongozi kama hawa, bado hamtafanikiwa malengo yenu.
Chagueni watu wenye malengo na mapenzi makubwa na klabu ili kuifanya Simba iwe mpya.
Mkifanya makosa, kumbukeni mtakuwa na safari nyingine ya miaka miwili.
Yapo mengi yanatakiwa kufanyika katika klabu, hivyo ni lazima kupata viongozi wenye mitazamo mizuri na uzalendo kwa timu.
Zipo changamoto za klabu, tafuteni watatuaji wa matatizo yenu na si watu wa kuongeza matatizo.
Kila la heri Simba katika usajili na uchaguzi wenu.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video