KOCHA wa timu ya taifa ya Colombia, Jose Pekerman amemtaja Radamel Falcao katika kikosi chake cha awali cha wachezaji 29 kwa ajili ya kombe la dunia nchini Brazil kuanzia mwezi ujao.
Nyota huyo wa klabu ya Monaco alikuwa katika hatihati ya
kushiriki kombe la dunia kutokana na kuumia vibaya goti lake kwenye
mchezo wa Coupe de France mwezi junuary mwaka huu.
Hata hivyo mwezi uliopita nyota huyo wa zamani wa Atletico
Madrid alisema anahitaji mwezi mmoja kuimarika zaidi, lakini Pekerman
ameamua kumujumuisha mshambuliaji huyo hatari.
Falcao alifunga mabao 9 katika mechi 13 za kuwania kufuzu kombe la dunia na alishirikiana vizuri sana na wachezaji,
Jackson Martinez na mchezaji wa Borussia Dortmund, Adrian Ramos.
Colombia wataanza kampeni zao za kombe la dunia katika kundi C dhidi ya Ugiriki Juni 14.
Kikosi kizima:
Walinda mango: Faryd Mondragon (Deportivo Cali), David Ospina (Nice), Camilo Vargas (Independiente Santa Fe)
Walinzi: Santiago Arias (PSV), Pablo Armero (Napoli), Eder
Alvarez Balanta (River Plate), Aquivaldo Mosquera (America), Luis Perea
(Cruz Azul), Carlos Valdes (San Lorenzo), Mario Yepes (Atalanta),
Cristian Zapata (Milan), Camilo Zuniga (Napoli)
Viungo: Abel Aguilar (Toulouse), Juan Cuadrado (Fiorentina),
Fredy Guarin (Inter), Victor Ibarbo (Cagliari), Alex Mejia (Atletico
Nacional), Juan Fernando Quintero (Porto), Aldo Ramirez (Morelia), James
Rodriguez (Monaco), Carlos Sanchez Moreno (Elche), Elkin Soto (Mainz),
Macnelly Torres (Al Shabab), Edwin Valencia (Fluminense)
Washambuliaji: Carlos Bacca (Sevilla), Radamel Falcao
(Monaco), Teofilo Gutierrez (River), Jackson Martinez (Porto), Luis
Muriel (Udinese), Adrian Ramos (Hertha Berlin)
Home
»
»Unlabelled
» RADAMEL FALCAO ATAJWA KIKOSI CHA AWALI CHA COLOMBIA KOMBE LA DUNIA
Wednesday, May 14, 2014
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment