Thursday, May 8, 2014


And now you've gotta believe us: Dzeko is joined by his City team-mates to celebrate his second goal
Dzeko akiungana na wachezaji wa Man City kushangilia bao lake la pili jana usiku
Acrobatic: City captain Vincent Kompany attempts an audacious overhead kick
Vitu vya hatari vya nahodha wa Man City Kompany
Can't even watch: Manuel Pellegrini can barely look with his side on the brink of a Premier League title
Hataki kutazama: Manuel Pellegrini yupo katika asilimia kubwa ya kutwaa taji la ligi kuu.
 
KOCHA wa Manchester City, Manuel Pellegrini amewasifu wachezaji wake kwa kuwa wavumilivu katika ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Aston Villa na kuukaribia ubingwa wa ligi kuu nchini Engalnd msimu.

Mabao ya kipindi cha pili yaliwahakikishia Man City ushindi na kurejea kileleni kwa pointi mbili mbele dhidi ya majogoo wa jiji, Liverpool,  huku wakisaliwa na mecho moja ya mwisho dhidi ya West Ham siku ya jumapili.

Vijana wa pellegrini walichanganyikiwa baada ya kuoneshwa upinzani mkubwa na Villa kipindi kizima cha kwanza, lakini dakika ya 64, Edin Dzeko alifunga bao la kuongoza na dakika nane baadaye aliongeza bao la pili.

Stevan Jovetic aliyetokea benchi aliihakikishia ushindi Man City baada ya kufunga bao la tatu dakika ya 86, kabla ya Yaya Toure kuhitimisha karamu ya mabao dakika za nyongeza.

Pellegrini ameipongeza timu yake kwa kucheza vizuri na kupata ushindi na sasa kuhitaji pointi moja tu kuchukua ubingwa kwasababu ya wastani mzuri wa magoli.

“Timu haikuvumilia tu, tulicheza vizuri”. Pellegrini ameiambia BBC Sport.

“Tulimiliki vizuri mpira. Tulijitahidi kukaa na mpira na kwenda mbele kwa kasi kadri tuwezavyo na tulitengeneza nafasi mbili au tatu kipindi cha kwanza”.

“Nilikuwa na uhakika kuwa kama tutaendelea kucheza vile tungepata nafasi za kufunga magoli”.

“Sasa tunaweza kuzungumzia ubingwa. Lazima tushinde mechi ya mwisho dhidi ya West Ham”.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video