MSHAMBULIAJI
wa zamani wa kimataifa wa England, Michael Owen anaamini Cristiano Ronaldo
ndiye mchezaji mkubwa zaidi kwa wakati wote katika klabu ya Real Madrid.
Ronaldo
amekuwa katika kasi kubwa msimu huu na kuvunja rekodi ya kufunga mabao mengi
zaidi katika msimu mmoja wa UEFA baada ya kupiga mawili katika ushindi wa mabao
4-0 dhidi ya Bayern Munich katikati ya wiki hii na kufikisha magoli 16.
Owen
aliyeichezea Real Madrid msimu wa 2004-05 amevutiwa na kiwango cha Ronaldo na
kuthubutu kusema kwasasa nyota huyo ni tunu ya klabu zaidi ya Ferenc Puskas.
“Nadhani
mchezaji mkubwa zaidi kwa wakati wote Real Madrid ni Cristiano Ronaldo
akifuatiwa na Ferenc Puskas”. Owen ameandika katika kolamu yake kwenye gazeti
la Sportlobster .
“Ronaldo
amelingana na Puskas” . amekuwa na rekodi kubwa ya mabao 242 katika mechi
chache.
“Pia
amekuwa mchezaji wa kwanza wa Real Madrid kufunga mabao 100 kwa haraka zaidi na
ameshikilia rekodi ya kuifungia Madrid mabao mengi zaidi ndani ya msimu mmoja”.
Pia
kwa kifupi, Owen alielezea maisha yake alipokuwa Real Madrid kuwa yalikuwa
mazuri kwa kazi yake hasa kwa vyombo va habari na mashabiki wake.
Michael Owen enzi zake akiwa Real Madrid |
“Sikuwa
na wasiwasi ya kutopata mafanikio katika uwanja maarufu.
“Nilikuwa
na mambo mawili: Nitafanya nini nitakaposhika mpira kwenye utambulisho wangu
Santiago Bernabeu na pili nitakaa wapi katika vyumba vya kubadilishia nguo”.
“Nilikuwa
katika wasiwasi mkubwa wakati wa utambulisho”.
“
Nilikuwa nafirikia maujanja ya kufanya nitakapotupiwa mpira.
“Nilionesha
ufundi mkubwa mbele ya vyombo vya habari na mashabiki waliokuwepo Bernabeu”.
“Hakukuwa
na jinsi ya kushindwa mbele ya vyombo vya habari vya dunia”.
Ghafla
Owen aliondoka Madrid ndani ya msimu mmoja akifunga mabao 14 tu katika mechi 36
za La Laiga alizocheza.
0 comments:
Post a Comment