Monday, May 12, 2014

SAM_1702


Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
Tel: 0712461976
KWA mara ya kwanza tangu Frank Domayo na Didier Kavumbagu waondoke kwenda Azam fc, mwenyekiti wa Young Africans, Yusuf Manji ameunguruma makao makuu ya klabu hiyo, makutano ya Twiga na Jangwani, Kariokoo jijini Dar es salaam.
Manji katika mazungumzo yake na waandishi wa habari jana alisema kuondoka kwa wachezaji wao wawili Kavumbagu na Domayo sio mwisho wa timu ya Yanga, kwasababu uongozi wake unaendelea na mipango ya kuhakikisha wanasajili wachezaji wengine wazuri kwa kufuata maelekezo ya Benchi la Ufundi.
Mwenyekiti huyo alisema yameongelewa mengi sana kwa kipindi cha mwezi mmoja ambao hakuwepo nchini kwa ajili ya kazi zake binafsi, lakini sasa amerejea na maandalizi ya msimu ujao yameshaanza.
“Kuondoka kwa Kavumbagu ni kutokana na kuchelewa kwa majibu ya TFF juu ya idadi ya wachezaji wa kigeni  kwa msimu mpya, huku Domayo ambae tangu mwaka jana aliombwa kuongeza mkataba alikua akisema anamsubiria mjomba wake ndipo aweze kufanya hivyo”. Alikaririwa Manji.
Kwa jinsi Manji alivyozungumzia suala la Domayo unagundua kabisa kwamba huyu jamaa ni mwepesi wa kukiri makosa. Ni jambo zuri kukubali makosa unapokuwa kiongozi. Kuna watu huwa hawawezi kikiri udhaifu kwa jambo lolote.
Hakuna mtanzania yeyote awe wanachama au si mwanachama wa Yanga asiyejua umuhimu na ubora wa Frank Domayo katika timu. Ni kijana mdogo mwenye kipaji cha hali ya juu na viongozi wa Yanga chini ya mwenyekiti wao Manji wanatambua hilo.
Baada ya kuondoka kwa Domayo, walisikika viongozi, wanachama na wapenzi wa Yanga wakisema Domayo si chochote. Lakini moyoni walikuwa wanaumia kwasababu wanajua ni mchezaji bora.
Wengi wao walikuwa hawakubali kufanya makosa zaidi ya kutamba kutafuta wachezaji wakali zaidi. Kwa bosi wao imekuwa tofauti kabisa, kwani ameanza kwa kukiri uzembe kufanyika, hivyo kujipanga upya.
Manji anajua kuwa viongozi wamefanya makosa kuondoka kwa Domayo, lakini haina jinsi kwasababu imeshatokea. Kwa maana nyepesi anawaomba radhi wanachama wa Yanga walioumia na kuondoka kwa nyota huyo. Njia ya kuwapooza ni kuwaletea wachezaji wengine watakaoziba nafasi ya kiungo huyo.
 Yangaleo1
Kwa suala la Kavumbagu, Manji amekuwa mkweli kuwa TFF ndio wamewayeyusha kwa kuchelewa kujibu juu ya sheria ya wachezaji wa kigeni. Hapa huwezi kuwalaamu sana, japokuwa kuna swali moja la kujiuliza, Azam walipokuwa wanamsajili Kabumbagu walijua kuwa sheria itabakia kuwa wachezaji watano?
Kama ndiyo, nani aliwaambia ? kwasababu walifikisha wachezaji 6 wa kigeni baada ya kumsajili Kavumbagu, lakini wakavunja mkataba na Ismail Kone na kubakia na watano.
Manji ameonesha ukomavu mkubwa wa uongozi, si mwepesi wa kuja juu, anapokosea anakiri na kuahidi kufanya vizuri zaidi. Kwa hili na ufafanuzi huu mzuri, Yufus Manji umepata kura yangu.
Pia Manji alisema pamoja na kuondoka kwa wachezaji hao bado kwa kushirikiana na kocha Hans der Pluijm watahakikisha Yanga inaendelea kutisha msimu ujao na kufanya vizuri kwenye mashindano ya kimataifa.
Pluijm wakati anaondoka wiki iliyopita aliahidi kuleta wachezaji wazuri watakaoisaidia Yanga .
Ni utaratibu wa makocha dunia kote kuwasilisha ripoti kila msimu unapomalizika.Yanga walishapokea ripoti ya Pluijm inayoeleza kila kitu.
Kwa kuzingatia mapendekezo ya mwalimu wao, Manji alisema wataleta `majembe` mapya ya kuisaidia Yanga katika mashindano ya msimu ujao wa ligi kuu na kombe la shirikisho.
Hapa lazima Yanga wasajili kwa kuzingatia mapendekez ya benchi la ufundi na si kusajili kwa sifa na kuwakomoa watu fulani.
Kombe la shirikisho ni mashindano makubwa, lazima wasajili vizuri kwa kuangalia nafasi na si kulundika wachezaji wasiokuwa na maana katika klabu kwa wakati huu.
Manji iambiea  kamati yako ya usajili na uwasimamie kuleta wachezaji hao unaoahidi kuwa watakuja kuziba nafasi za Domayo na Kavumbagu.
Suala la ujenzi wa Uwanja wa Kisasa eneo la Jangwani , Manji alisema bado lipo pale pale, kikubwa kinachosubirwa ni majibu ya serikali juu ya maombi ya eneo la ziada, kwani Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam alisema suala hilo lipo ukingoni na mda si mrefu.
Simba na Yanga zinatia aibu kwa hili la kukosa viwanja. Kuna wakati timu hizi zinahangaika kutafuta wapi kwa kufanyia mazoezi.
Wakati fulani Mahafali ya kidado cha nne au saba inavunja program ya mazoezi ya klabu hizi kwasaabu viwanja wanavyoomba hutumika kwa sherehe. Aibu iliyoje hii.
Hii ni fedheha kubwa sana kwa timu hizi kongwe katika soka la Tanzania.
Siku za karibuni, aliyekuwa makamu mwenyekiti wa Yanga miaka ya nyuma, Bilionea Davis Mosha alikaririwa akisema anashangaa kuona Azam fc iliyokuja juzi juzi tu ikishindana na Yanga kupora wachezaji.
Mosha alijenga hoja yake kuwa Yanga ni klabu kongwe ambayo inastahili kuchukua wachezaji Azam fc na si Azam kuchukua Yanga. Suala la Domayo lilimuuma sana Mosha na kuamua kufichua ya moyoni.
Mosha aliwalaumu viongozi kwa kufanya uzembe wa kuwaachia wachezaji hawa. Na jana Yusuf Manji alikiri kuzembea juu ya suala hili.
Pia Mosha alisema klabu ya Azam fc iliyokuja juzi inamiliki uwanja, TV na sasa wanajiandaa kuanzisha redio yao. Bilionea huyo alisikitika sana.
Suala la uwanja si Mosha peke yake, wapenzi wengi wa soka wanazishangaa Yanga na Simba kushindwa kujenga hata viwanja vya mazoezi.
 10
Tatizo kubwa ni siasa kutawala kwa viongozi wa klabu hizi. Wamekuwa wakiahidi kujenga viwanja, lakini inapofika utekelezaji wanakula kona.
Aden Rage wakati anaingia madarakani katika klabu ya Simba miaka miwili iliyopita, aliahidi kupambana na kujenga uwanja wa kisasa. Lakini baadaye alikuja kuruka kamba na kusema kama serikali ya CCM imejenga uwanja wa Taifa kwa miaka 50, yeyee na kamati yake wanawezaje kujenga uwanja kwa miaka miwili?
Swali, wakati anaingia madarakani hakujua kama kujenga uwanja ni gharama kubwa?, na kwanini aliahidi wakati anajua hawezi. Hizi ndio siasa za mpira wa Simba na Yanga.
Miaka miwili sasa imepita,  Yusuf Manji aliahidi kujenga uwanja wa kisasa katika klabu ya Yanga. Muda wake umeisha na hatagombea tena, huku dalili za kujenga uwanja zikiwa hazionekani.
Viongozi wa Yanga mara zote wamekuwa wakishindwa kunyosha maelezo juu ya ujenzi wa uwanja mpaka sasa wanaondoka madarakani.
Maneno ya Manji hapo jana kuwa ahadi ya uwanja ipo palepale ni kutoka mdomoni tu, utekelezaji unasubiriwa kwa hamu. Si mara ya kwanza kwake kutamka juu ya hili, na watu tunakumbuka alishawahi kusema.
Kwasasa hatuna haja ya kusikia akisisitiza ahadi yake bali tunataka kuona vitendo. Kusema ahadi ipo palepale ni maneno ya siasa tu, kisayansi hatujaona kitu chochote katika ahadi hiyo.
Kama kweli Bilionea huyo anataka kujenga uwanja , basi kuna haja ya kuungana na wenzake kuhakikisha wanatekeleza ahadi hii tamu kwa wanayanga.
Yanga ina rasilimali nyingi na mtaji mkubwa wa wanachama nchi nzima. Kuna kila uwezekano wa kufanikisha ujenzi wa uwanja, lakini tu kama watapatikana viongozi wenye mtazamo wa maendeleo.
Kuelekea uchaguzi ujao, wanachama wa Yanga chagueni watu watakaoshirikiana na mwenyekiti wenu atakayekuwa mstaafu kwa wakati huo, Yusuf Manji ili mjenge uwanja wenu.
Igeni mfano wa Azam fc ambao hutumia zaidi vitendo na si siasa za kupeana moyo kila wakati. Tutajenga uwanja tutajenga uwanja sasa imekuwa kama wimbo wa taifa.
Kwa Manji kulifuta rasmi tawi la Tandale kutokana na kuwa na chanzo cha vurugu na migogoro ndani ya klabu, pia amewafuta uanachama wanachama sita ambao walikiuka katiba ya Yanga kwa kwenda kuongea na waandishi na HABARI bila ya Idhini ya uongozi huku pia wakishindwa kulipia ada zao za uanachama kwa zaidi ya miezi sita, sina tatizo nalo.
Kama waliunda wenyewe sheria hiyo na kuambizana, basi watajijua wao wenyewe. Kuvunja sheria mliyojiwekea wenyewe kwa matakwa yenu ni makosa na halina maswali.
Kuongea na vyombo vya habari sio kosa kwasababu ni haki ya kikatiba, lakini kama kuna sheria ambayo Yanga wamejiwekea kwa kukubalina, basi sisi tuliopo nje ya Yanga hatuna maswali. Waliofutwa uanachama ni:
1. Ally Kamtande, 2. Isiaka Dude, 3. Hamisi Matandula, 4.Waziri Jitu Ramadhani, 5.Mohamed Kigali Ndimba , 6. Selaman Hassan Migali 
Mkutano mkuu wa mabadiliko ya katiba utafanyika terehe mosi Juni, 2014 katika Ukumbi wa Oysterbay Police Mess na wanachama wote wanaombwa kulipia ada zao ili waweze kuhuhudhira mkutano huo wakiwa hai. 

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video