Saturday, May 10, 2014



 Aguero: I’ll play through the pain against West Ham
 MSHAMBULIAJI wa Manchester City, Sergio Kun Aguero kwa asilimia 100 anaamini atacheza mechi ya mwisho ya ligi kuu soka nchini England jumapili dhidi ya West Ham, hata kama atakuwa na maumivu.
Nyota huyo raia wa Argentina alipata majeruhi kwenye mechi dhidi ya Everton na kukosa mechi ya katikati  ya wiki dhidi ya Aston Villa ambayo City walishinda mabao 4-0. 
Wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa yanawafanya City wahitaji sare ili kutwaa ubingwa, huku Aguero akisema lazima achangie ushindi Etihad jumapili.
“Najisikia vizuri- lakini kwa asilimia 100 siko fiti,  jumapili lazima nicheze,” nyota huyo mwenye miaka 25 ameiambia tovuti ya klabu.
“Hata kama sitakuwa fiti, umuhimu wa mechi hii ambayo kila mtu anatamani kucheza utanifanya niingiae uwanjani na sitasikia maumivu”.
Aguero sio mgeni katika kuamua matokoe kwa mechi za mwisho na msimu wa 2011/2012 alifunga bao lililowapa ubingwa Man City dhidi ya QPR, lakini nyota huyo amesema West Ham hawatakuwa sawa na QPR waliokuwa wanapambana kukwepa kushuka daraja.
“Nadhani itakuwa tofauti, lakini haimaanishi itakuwa kazi rahisi”. Aliendelea.
“Wana nguvu nzuri-West Ham wanakuja Etihad kwa malengo ya kutufunga, lakini hawana presha yoyote, kwahiyo mechi itakuwa tofauti”.

“Sisi tuko katika presha ileile kama wakati ule kwasababu tunahitaji kushinda ili kutwaa ubingwa”

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video