MSHAMBULIAJI wa Barcelona, Mbrazil, Neymar,
amesema anafurahia mahusiano yake mazuri na mchezaji mwenzeka wa klabu hiyo,
Lionel Messi.
Bosi wa Barca, Gerardo Martino Tata ameshindwa
kuwatumia wawili hao kama ilivyotarajiwa kutokana na kukumbwa na majeruhi ya
mara kwa mara msimu huu.
Kumekuwepo na taarifa kwenye vyombo vya habari
kuwa wawili hao hawana mahusiano mazuri na hawataki hata kuonana ana kwa ana, lakini
Neymar amesisitiza kuwa yeye na Messi ni marafiki wakubwa ndani na nje ya
uwanja.
“Hatuchezi wote kila mchezo, lakini nadhani
tumejenga uhusiano mzuri tena wakustaajabisha”. Nyota huyo wa kimataifa wa
Brazil amesema wakati wa mahojiano na CNN.
“Watu wengine walisema tusingeelewana, lakini
ulikuwa uongo. Ni mtu rafiki sana, ni nyota ninayempenda”.
Neymar alicheza katika fainali ya Copa del Rey
aprili 16 mwaka huu ambapo Barcelona walicharazwa mabao 2-1 na Real Madrid ,
lakini alipata majeruhi na ilithibitishwa kuwa atacheza fainali za kombe la
dunia majira ya kiangazi mwaka huu nchini kwake Brazil.
Neymar aliongeza: “Nitakuwa fiti kwa fainali za
kombe la dunia. Tatizo pekee ni kwamba siwezi kuisaidia Barcelona. Natarajia
kubeba kombe la dunia na nitawasaidia wenzangu kutimiza malengo haya”.
“Najua wajibu wangu kwa timu yangu ya taifa, kama
ilivyo kwa wenzangu. Tumekuwa wamoja na tutasaidiana sana, tunajiandaa kutwaa
taji la kombe la dunia”.
Mbrazil huyo pia ametumia nafasi hiyo kueleza
masikitiko yake juu ya utata wa uhamisho wake uliofanyika mwezi juni mwaka jana kutoka klabu yake ya
zamani ya Santos kujiunga na Barca.
“Kila kitu kilikuwa sahihi na hatukufanya makosa
hata kidogo”. Neymar aliendelea.
“Jinsi ambavyo Santos walilichukulia suala langu
waliniacha katika huzuni, lakini nitafanya nini”
“Siwezi kuwajibia, lakini nazungumza kivyangu na
kwa ajili ya baba yangu kwamba hatua walizotaka kuchukua kutatua tatizo hili
hazikupendeza”.
0 comments:
Post a Comment