Thursday, May 15, 2014

_DSC0696 
Na Baraka Mbolembole Kuna watu wamezaliwa kuwa viongozi, kila wanachokuwa wanasimamia huendavizuri. Jana ndiyo ilikuwa siku ya mwisho kwa wanachama wa klabu ya soka ya Simba kuchukua na kurudisha fomu za kuwania nafasi za urais, makamu wa rais wa klabu na wajumbe wa kamati ya utendaji. Siku ya jana niliandika makala kuhusu mtu anayepaswa kuwa rais wa klabu hiyo anavyotakiwa kuwa. Leo, nitazungumzia kidogo kuhusu nafasi ya umakamu wa rais ambayo wanachama watano wamechuku fomu za kugombea nafasi hiyo. Wanachama wawili kati yao walikuwepo katika utawala unamaliza muda wake, Geofrey Nyange Kaburu ambaye katika kipindi cha miaka ya uongozi unamaliza muda wake alikuwa ni makamu mwenyewe, kabla ya kujiuzulu mapema mwaka 2013, na Joseph Itangare ‘ Mzee Kinesi’ ambaye alikaimu nafasi iliyokuwa imeachwa na Kaburu kwa muda wa mwaka mmoja na nusu. Wamefuata nini tena? Wameongeza ujuzi gani katika fikra zao za utawala? Wanarudi, Simba kufanya nini?
Jana nilimsikia aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Jamhuri Kihwelo akitoa yake ya moyoni ambayo yamemfanya kuchukua fomu za kugombea nafasi ya umakamu wa rais. Unafikiri, Julio alikuwa pale kuwachekesha watu na kutengeneza vichwa vya habari katika media, hapana. Nafikiri ameguswa na orodha ya wagombea waliojitokeza kuwania nafasi hiyo. Kwa mtu anayeifahamu, Simba nje-ndani kama, Julio bila shaka atakuwa tayari kutoka nje ya taaluma yake ya ukocha na kwenda kujaribu kuokoa jahazi katika nafasi ya uongozi katika timu anayoipenda na kuishabikia.
Kama atafanikiwa kushinda kama alivyodai yeye mwenyewe, upande wangu nitakuwa na mashaka na wapiga kura, ila sitashangaa endapo wanachama watampeleka madarakani. Kuna vitu vinachosha, na kuna watu hawataki kukubali matokeo ya kushindwa wakati ni changomoto tu katika harakati za maisha. Samahani, nauliza tu, hivi watu kama Kaburu na Itang`are wanarudi Simba kufanya nini?. Kama tunawahitaji kina, Issa Hayotou katika klabu zetu na tuwarudishe madarakani sasa! Si, tunawapenda! Tunawaheshimu! Tunawanyenyekea! Hatuna kitu bila wao! Upande wangu napenda kuwafagilia na kuwaunga mkono viongozi wenye sera na mitazamo ya kisasa yenye maendeleo hata kama watakuwa wapenda madaraka kama, Sepp Blatter. Unaweza kuwa na tamaa ya kuongoza jambo au taasisi Fulani lakini katika njia ya kufikia tamaa hiyo ukawa unakutana na vikwazo vingi kitu ambacho kinakufanya ujifunze zaidi. Kwa, mfano, mimi ningewaambia, Itangare na Kaburu wakajifunze kwanza jinsi ya kuunganisha mahusiano ya kiutawala kati ya kiongozi wa chini na Yule wa nafasi ya juu. Wote hawa walishindwa kwenda sambamba na mwenyekiti anayemaliza muda wake, Mh. Aden Rage. Nakumbuka kuna wachezaji wengi waliwahi kuniambia kuhusu kutothaminiwa, kunyanyaswa katika malipo, na kudharauliwa na makamu huyo mwenyekiti wa zamani aliyejiuzulu katika utawala unaomaliza muda wake. Upande wa Itangare, yeye ni mtu muhimu na ambaye ameisaidia sana Simba, kifedha na ki-hali, ila ni mtu dhaifu katika mambo ya utawala. Anayumba, kama vile bendera inayofuata upepo. Sijui sana kuhusu wao, ila kiutawala ni watu ambao naweza kuwaongea na kuwashauri.Wangejifunza kwanza ili kuwa viongozi makini, muda bado upo, Simba itaendelea kuwepo.Simba inatakiwa kuwa na rais na makamu wake wenye mtazamo sawa. Sifikirii kama safu ya Michael Wambura na Itangare, Swed Nkwabi au Kaburu inaweza kutoa mafanikio mazuri. Watakuwa wakipishana tu, kama ilivyokuwa kwa Aden Rage. Sijui kwanini ila nipo njiani kupata ukweli wake. Julio, amekumbusha hadi madeni yake ya wakati wa uongozi wa Mzee, Hassan Dalali. Amesema viongozi wanaomaliza muda wao katika utawala wa sasa hawapaswi kupewa nafasi safari hii. Akaongeza, yeye ni kocha wa Simba hadi leo hii. Hahaha, Julio ukimuona anaongea kama anaropoka jua kuna ukweli hapo. Ujumbe umefika, nafikiri huyo ni bora zaidi katika nafasi ya umakamu wa rais katika klabu ya Simba, kama watashindwa kuwatazama usoni. Katika kazi za kimagereza, mfungwa unapatiwa kazi, ukiwa nyuma wewe ni mvivu, utapigwa kweli, ukiwahi utaambiwa unataka kutoroka! Mfungwa anafanya kazi kwa saa, anakula kwa wakati maalumu, kulala muda uliopangiwa na kuishi katika taratibu za kimagereza. Nafasi ya makamu wa rais, Simba SC, haina watu sahihi? Julio, ameshazungumza kuwa anaidai, Simba, sijui atajilipa kwanza madeni yake akiingia madarakani? Huyu amechoshwa na mengi ndani ya Simba, anataka viongozi makini, wasio wanyonyaji, wenye uchu na moyo waki-Simba hasa. Yeye ndiye, kwa waliopo! Kutoka uchezaji, ufundishaji, hadi umakamu wa rais, Simba SC, Julio ni mtu jasiri, nazisubiri, rufaa zake! Nakumbusha tu, vita ya kwanza kubwa ya viongozi wajao ni kuvunja utegemezi kutoka kundi la marafiki wa Simba. Nimewasilisha tu, kesho tena, Inshallaha! 0714 08 43 08

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video