Mwanasheria na wakala wa wachezaji FIFA, Dkt. Damas Ndumbaro
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
KUFUATIA uongozi wa Azam fc kumsainisha mkataba wa
miaka miwili kiungo mkabaji wa Yanga sc, Frank Domayo `Chumvi` akiwa katika kambi ya Taifa ya Tanzania,
mwanasheria na wakala wa kimataifa wa
wachezaji anayetambuliwa na shirikisho la soka duniani FIFA, Dkt. Damans
Ndumbaro amesema hakuna sheria inayozuia mchezaji kusainishwa mkataba akiwa
kambi ya timu ya Taifa.
Akizungumza na mtandao huu, Ndumbaro amesema
sheria inaeleza kuwa mchezaji anayetakiwa kusajiliwa na timu ni yule aliye huru baada ya kubakiza miezi
sita katika mkataba wake au ana mkataba, lakini klabu inayomhitaji imezungumza
na timu inayommliki mchezaji.
“Domayo ni
mchezaji huru na alikuwa huru kwenda klabu yoyote”. Alisema Ndumbaro.
Pia alisema hakuna sheria inayosema kambi ya timu
ya Taifa ni eneo linalozuiliwa watu kwenda.
“Kambi ya timu ya Taifa watu huwa wanaenda.
Kumbuka Yondani alisajiliwa Yanga akiwa timu ya taifa, na hatukusikia mzozo
wowote kwasababu hakuna kununi inayozuia hilo”.
“Kama mchezaji ametoroka kambini ataadhibiwa kwa
utoro, lakini kambi ya timu ya taifa ni sehemu ya wazi na watu wanaruhusiwa kwenda
pale na huwezi kukataza watu kwenda pale”
“Kumbuka timu inakaa hotelini na hoteli huwa
hawakai wachezaji tu, kila mtu anaweza kukaa pale”. Alisema Ndumbaro.
Kutokana na tukio
lililotokea Aprili 30 mwaka huu kwenye kambi ya timu ya Taifa (Taifa Stars)
iliyopo Tukuyu mkoani Mbeya likihusisha usajili wa Frank Domayo, Rais wa
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amemteua Wakili
Wilson Ogunde kuchunguza mlolongo mzima wa tukio hilo.
Baada ya kukamilisha
uchunguzi wake, Wakili Ogunde ataishauri TFF kuhusu hatua za kisheria na
kikanuni za kuchukua.
TFF ilitoa wito kwa
wachezaji, klabu na wadau wa mpira wa miguu kufuata kanuni na taratibu katika
utendaji wao.
0 comments:
Post a Comment