Bosi wa Chelsea Jose Mourinho anaamini Eden Hazard hayuko tayari kujitolea kwa ajili ya timu.
Jose Mourinho amejibu mapigo kwa winga
wake Eden Hazard aliyekosoa mbinu zake za ufundishaji wa mpira kwa
kueleza kuwa winga huyo wa Chelsea kwa asilimia 100 hajitolei kwa ajili
ya klabu yake.
Bosi huyo wa
Chelsea ameanza mkutano wake na waandishi wa habari mchana wa leo kwa
kumtetea Mbelgiji huyo kwa maneno aliyokaririwa na vyombo vya habari kwa
kufafanua kuwa maneno ya Hazard `yalibadilishwa`, lakini Mourinho
alihitimisha kwa kusema kuwa hakumfurahia winga huyo.
. "Hakunikosoa. Ni
kawaida kupata maoni kwa wachezaji kama yeye ili kutatua matatizo kama
tuliyokuwa nayo katika goli la kwanza dhidi ya Atletico"
"Mechi
ya kwanza ya UEFA, Willian alicheza winga ya kushoto na kumsaidia sana
Cole. Eden ni mchezaji ambaye hana akili ya kumwangalia beki wake wa
kushoto".
Hazard (kushoto) alikaririwa akisema Chelsea hawafundishwi soka la kisasa
Mourinho pia anaamini maneno ya Hazard juu ya mbinu zake za ufundishaji yamebadilishwa na vyombo vya habari
0 comments:
Post a Comment