Saturday, May 3, 2014



9fd3Zacharia-Hans-Poppe
Zacharia Hans Poppe amezikaribisha klabu zenye dau nono kumendea wachezaji Simba

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
KAMATI ya usajili ya klabu ya Simba SC inatarajia kukutana jumatatu ya wiki ijayo kujadili ripoti ya kocha mkuu, Mcroatia, Dravko Logarusic  tayari kwa mikakati ya msimu ujao.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Keptein wa zamani wa Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ), Zacharia Hans Poppe  ameuambia mtandao huu jioni hii kuwa malengo ya Simba ni kuimarisha kikosi chao, hivyo wanaanza mikakati rasmi jumatatu kwa kupitia mapendekezo ya Loga juu ya wachezaji atakaondelea nao na wachezaji gani wasajiliwe.
“Tutakutana rasmi jumatatu na kufikia jumatano ya wiki hiyo hiyo tutakuwa tumehitimisha kuijadili na kuanza harakati za kutekeleza yaliyomo”. Alisema Poppe.
Mwanajeshi huyo wa zamani wa JWTZ aliongeza kuwa kuna wachezaji muhimu watakaobakishwa kwasababu wana mikataba na Simba, hivyo hakuna klabu itakayowasajili bila maridhiano na Simba sc.
“Tambwe anahusishwa kuondoka,lakini ana mkataba wa mwaka mmoja na sisi. Kwahiyo kama mtu anataka kuzungumza naye sheria inambana na lazima aje kuzungumza na  Simba”.
“Wachezaji wote tunaohitaji kuendelea nao wana mikataba na Simba. Kuna wengine ni mwaka mmoja, wengine miwili hadi mitatu”.
“Mfano Jonas Mkude, Ramadhan Singano  wanamaliza mikataba yao 2017.
“Wachezaji wote wanaohusishwa kuihama klabu wana mikataba mirefu na sisi”. Aliongeza Poppe.
Aidha, Poppe alisema hakuna mtu aliyeenda rasmi kuzungumza na Simba mpaka sasa, lakini wakifika, Simba haina tatizo kwani si utaratibu wake kuwazuia wachezaji kuondoka.
“Hata kama mchezaji yupo katika mipango ya mwalimu, lakini timu ikataka nyingine ikahitaji kumsajili, sisi tunamruhusu na kutafuta mwingine”.
“Ukipata dau nono unatafuta mchezaji mwingine na unaweza kuambulia na faida kwa manufaa ya klabu”. Alisema Poppe.
Poppe aliwaondoa hofu wanachama na mashabiki wa Simba kwasababu safari hii wanakwenda vizuri na wataanza msimu mpya kwa kasi nzuri.
Simba sc ilimaliza msimu uliopita kwa kushika nafasi ya 4 kwa pointi 38, huku nafasi ya tatu ikishikwa na Mbeya City, ya pili Yanga na Azam fc ndio walikuwa mabingwa.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video