Na Baraka Mpenja, Dar es Salaam
0712461976
Shirikisho la soka Tanzania TFF limetangaza
kuwa ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuanzia msimu wa 2015/2016 itakuwa na timu 16
badala ya 14 za sasa.
Afisa habari wa TFF, Boniface Wambura katika taarifa yake kwa vyombo vya habari mchana huu ameseme mabadiliko hayo yamepitishwa na Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana jana (Mei 3 mwaka huu) jijini Dar es Salaam baada ya kupokea mapendekezo ya kuongeza idadi ya timu kutoka kwenye Kamati ya Mashindano.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa uamuzi huo umefanywa kwa lengo la kuongeza ushindani katika ligi hiyo, na kuwezesha wachezaji kupata mechi nyingi zaidi za mashindano.
Afisa habari wa TFF, Boniface Wambura katika taarifa yake kwa vyombo vya habari mchana huu ameseme mabadiliko hayo yamepitishwa na Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana jana (Mei 3 mwaka huu) jijini Dar es Salaam baada ya kupokea mapendekezo ya kuongeza idadi ya timu kutoka kwenye Kamati ya Mashindano.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa uamuzi huo umefanywa kwa lengo la kuongeza ushindani katika ligi hiyo, na kuwezesha wachezaji kupata mechi nyingi zaidi za mashindano.
Kwa mabadiliko hayo maana yake ni kuwa Ligi ya
msimu wa 2015/2016 itakuwa na mechi 240 wakati kwa sasa ina mechi 182.
Mtandao huu umebahatika kukutana na makocha na
wachambuzi wa soka ili kupata maoni yao, baadhi yao ni hawa hapa chini.
Ally Mayay Tembele ( waliochuchumaa, wa pili kushoto) enzi zake akiichezea Yanga
ALLY
MAYAY TEMBELE-Beki na nahodha wa zamani wa Yanga, kwasasa kocha na mchambuzi wa
soka.
Kwa upande wake amesema: “Siku zote tulitaka
hivyo, tulitaka idadi ya timu za ligi kuu iongezeke sio leo wala jana”.
“Tangia mkataba wa kwanza wa Vodacom tulizungumza
kwamba nia yetu ni kuwa na timu 18, mimi nilicheza ligi ya timu 18 miaka hiyo.”
“Timu 14 ni chache hakuna anayepinga hilo, binafsi
napongeza mabadiliko.”
“Angalizo ni kwamba tusije tukawa ni timu
zinazokuja kushiriki ligi, tupate timu zinazokuja kushindana, tupate timu kama
Mbeya City fc ambazo kweli zinakuja kushindana na sio kuongeza timu zinazokuja
kushiriki, hapo tutakuwa hatujafanya kitu”.
“Nashauri pia mashindano mengine yarudishwe
kwasababu ni ukweli kwamba ili mchezaji awe bora, kwa mwaka anatakiwa kucheza
mechi si chini ya 40 au 50”.
“Uingereza mchezaji anacheza mechi mpaka 60, hapa
kwetu mchezaji anacheza mechi 26 za ligi kuu, hatuwezi kukuza kiwango cha
mchezaji kwa mechi chache hizi.”
KENNEDY MWAISABULA `MZAZI`- kocha wa mpira wa
miguu aliyewahi kuzifundisha timu mbalimbali za ligi kuu ikiwemo Yanga sc.
Yeye amesema: “Kwanza nawapongeza TFF kwasababu
ndio kilio cha watanzania wengi kwamba timu ziongezeke, tena si 16 bali zifike
mpaka 20 na ndio lengo la watu wengi”.
“Ili soka la nchi likue lazima wachezaji wawe na
mechi nyingi, kwahiyo naipongeza kamati ya TFF kuliona hilo, lakini bado kuna kazi
ya kuongeza mpaka zifike 20”.
“Mwaka 2001 wakati nafundisha Bandari FC ya
Mtwara, timu zilikuwa 24 na usafiri wa kwenda Mtwara ulikuwa unachukua zaidi ya
siku tatu, lakini bado kulikuwa na ligi ya aina hiyo”.
“Leo ukitaka kwenda Mtwara inachukua siku moja,
ukitaka kwenda Mwanza ni siku moja, kwahiyo nasema tunahitaji kuwa na timu 20 kama
nilivyosema, lakini napongeza kwa hizo mbili zilizoongezwa kuwa 16”.
“FIFA wanakwambia ili mchezaji afikie kiwango cha
juu anatakiwa kucheza mechi 40 kwa mwaka”.
“Mashandano mengine kama ligi ya muungano, Kombe
la FA, kombe la Taifa yarudishwe, kama FA itakuwepo na mimi nitaingiza timu yangu
ya Maji Matitu, hahahah!”.

FREDY FELIX MINZIRO- Kocha wa JKT Ruvu, lakini kwa
muda mrefu amefanya kazi na Yanga sc.
Kwa upande wake yeye amesema: “Kama wameongeza
timu, basi na maeneo mengine kama udhamini, maamuzi vifanyiwe kazi”.
“Kuongeza timu ni jambo zuri na wachezaji watakuwa
na mechi nyingi, hivyo ligi itazidi kuwa na ushindani”.
“Kila timu itakuwa imejiandaa kivyake, lakini
wadhamini wa ligi kama Vodacom, Azam watatakiwa kutoa fedha kwa wakati muafaka
ili timu zote zijiandae vizuri”.
“Timu zinapokuwa nyingi, mambo ya udhamini nayo
yaende sambamba, wakichelewesha timu zitatofautiana kimaandalizi”.
Mtandao huu unaendelea kuzungumza na wadau na
makocha wa soka mbalimbali, nini maoni yako msomaji wetu mpendwa?.
0 comments:
Post a Comment