Matatani: Anara Atanes anakabiliwa na kesi kwa kumtusi kocha wa Ufaransa, Didier Deschamps
KOCHA
timu ya taifa ya Ufaransa, Didier Deschamps amefungua kesi dhidi ya mpenzi wa Samir Nasri aliyemtusi
mwalimu huyo baada ya kutaja kikosi cha Ufaransa cha Kombe la Dunia na kumtema kiungo huyo nyota wa Manchester City.
Anara Atanes aliposti kwenye akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Twitter- matusi haya; "F*** France and F*** Deschamps! What a s*** manager".
Lakini ingawa baadaye aliomba radhi, Deschamps atachukua hatua za kisheria dhidi ya Atanes.
Kituo
cha Redio cha Ufaransa, RMC kimeripoti kwamba Deschamps na Shirikisho
la Soka Ufaransa (FFF) wote wamefungua kesi dhidi ya Atanes, ambaye ni
mzaliwa wa England na mwimbaji wa kundi la Pop, Fanfare.
0 comments:
Post a Comment