KOCHA
wa Barcelona, Gerardo Martino amesema kamwe tetesi zinazoendelea juu ya hatima
yake haziwezi kuathiri kazi yake wakati huu akifukuzia ubingwa wa La Liga.
Barca
walipoteza matumaini ya kubeba makombe matatu msimu huu mwezi uliopita baada ya
kufungwa fainali ya copa del Rey na kutolewa UEFA na sasa wamebakiwa na
matumaini ya ubingwa wa ligi kuu pekee.
Wakatalunya
wapo nyuma pointi nne kwa vinara wa La Liga, Atletico Madrid.
Martino
amekuwa katika hatari ya kupoteza kazi, huku Michael Laudrup na Roberto Martinez
wakihusishwa kutwaa kibarua hicho, lakini Margentina huyo amekiri kuwa msimu
huu umekuwa mgumu kwake.
“Kwasasa
nafikiria mechi mbili zijazo ambazo zinaweza kuamua kama bado tutaweza kubeba
taji la La Liga”. Martino amewaambia waandishi wa habari leo hii ijumaa.
“Kuhusu
tetezi za kuachishwa kazi, kiukweli haziniathiri, ninachoangalia kwasasa ni
matokeo, majina ya watu wa kunirithi nayasikia, lakini hayaniathiri”.
“Mimi
na klabu hatujakaa kuzungumza lolote, hakuna haja ya kuniuliza kama nitaendelea
kuwepo kwasababu mkataba wangu bado ni hai sana”.
Wakatalunya
kesho jumamosi wanavaana na Getafe, lakini Martino hajaathiriwa na tetesi
zinazomkabili kwa sasa.
“Ni
kweli Getafe wanapigana kupata nafasi nzuri, lakini klabu zote zinapigana
kupata kitu fulani. Tutacheza vizuri, sio mchezo wa kesho tu bali ni mechi zote
zilizosalia kumaliza msimu”.
Elche
na vinara Atletico ndio wapinzani wa Barcelona katika mechi zao mbili za
mwisho.
0 comments:
Post a Comment