KOCHA
wa Everton, Roberto Martinez amekanusha taarifa kuwa klabu yake ina mpango wa
kuwaachia Manchester City katika mchezo wao wa jamamosi wiki hii ili kuwanyima
nafasi ya kutwaa ubingwa wa ligi kuu nchini England wapinzani wao wa jadi,
Liverpool msimu huu.
Taarifa
zilizozagaa kwa sasa zinaeleza kuwa mashabiki wa Everton watakuwa na furaha
kama klabu yao itafungwa na vijana wa Manuel Pellegrini ili kuwanyima ubingwa
mahasimu wao wa Merseyside ambao kwa miaka 24 wamekuwa katika ukame wa mataji.
Lakini
Martinez amekanusha na kusema wachezaji wake hawawezi kushawishika kirahisi na
watajitahidi kwa uwezo wao wote kuwafunga Man City, ikizingatiwa bado wana
matumaini finyu ya kufuzu UEFA mwakani.
“Sina
wasiwasi na klabu yangu katika mashindano ya ligi. Sisi ni klabu ya mpira wa
miguu na tunahitaji kushinda kila mchezo uliopo mbele yetu”
“Kuiachia
timu nyingine” hapana! Huwa hatufanyi kazi kama hiyo. Tutajitahidi kushinda
kila mchezo na tuko katika kiwango kizuri. Tunaiwakilisha vizuri klabu yetu”.
“”Kamwe
hatutaweza kumzawadia mtu ushindi. Hatuibebi klabu yoyote”.
Kocha
huyo wa zamani wa Wigan pia ameeleza kuwa mchezaji wake Phil Jagielka
atajumuishwa katika kikosi cha jumamosi, wakati Sylvain Distin naye atakuwa
tayari kurudi uwanjani.
0 comments:
Post a Comment