KOCHA
wa Everton, Roberto Martinez ameomba sheria ya wachezaji wa mkopo ifanyiwe
marekebisho na kuwaruhusu kucheza dhidi ya klabu walizotoka.
Martinez
ameweza kuwatumia vizuri wachezaji wake wa mkopo akiwa Goodison Park, Romelu
Lukaku, Gerard Deulofeu na Gareth Barry na wote wamekuwa katika kiwango cha kuvutia
katika klabu hiyo ya Merseyside.
Kocha
huyo atamkosa Barry jamamosi kwenye mchezo dhidi ya Manchester City kwasababu
sheria ya mkopo haimruhusu kucheza na klabu yake inayommiliki.
Kocha
huyo wa zamani wa Wigan Athletic amesema imefika wakati watu wa sheria za ligi
kuu nchini England waliangalie hilo, huku akionesha mfano jinsi Atletico Madrid
walivyomtumia Thibaut Courtois dhidi ya mwajiri
wake wa kudumu, klabu ya Chelsea kwenye mechi za nusu fainali za UEFA.
“Unapofikia
makubaliano ya kumtoa mchezaji kwa mkopo, aruhusiwe kucheza”. Martinez alisema.
“Sioni
kama ni haki kumnyima mchezaji haki ya kucheza na klabu yake aliyomwajiri”.
“Ni
haki kufanya kama ilivyo katika mashindano ya ulaya, kumuona mchezaji akicheza
na timu yake iliyomwajiri ni jambo zuri na nadhani itakuwa jambo la maana na
baada ya msimu ataangaliwa kiwango chake”.
“Sheria
ya mkopo inahitaji mabadiliko ili kuendana na soka la kisasa. Ni mjadala mzuri
na ni jambo la kuangaliwa kwa ndani”.
“Hatupaswi
kuwa na sheria mbili tofauti katika mashindano. Nadhani sheria za ligi ya ndani
ziende sambamba na sheria michuano ya ulaya”.
0 comments:
Post a Comment