KLABU ya Manchester City inatumai kumalizia makubaliano ya vipengele via mkataba na beki wa Arsenal, Bacary Sagna baada ya fainali ya Kombe la FA.
Beki huyo wa kuli amekuwa katika mvutano wa kusaini Mkataba mpya na klabu yake ya sasa juu ya mshahara mpya anaoutaka wa Pauni 100,000 kwa wiki.
Mkono wa kwaheri: Bacary Sagna, akiwa Uwanja wa Emirates wiki iliyopita, anatarajiwa kuondoka Arsenal mwishoni mwa msimu
Bodi ya The Gunners sasa tayari imemuambia Sagna hawawezi kumpa kiwango hicho cha mshahara, manna ale huo ndiyo mwisho wake Arsenal.
Sagna amekuwa beki wa kwanza wa kulia kwenye kikosi cha Arsene Wenger, kinachotarajiwa kumenyana na Hull City kesho katika fainali ya Kombe la FA.
0 comments:
Post a Comment