Damas Ndumbaro |
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
MWENYEKITI wa kamati ya uchuguzi ya Simba sc,
Damas Ndumbaro anatarajia kukutana na waandishi wa habari kesho na kuweka
hadharani majina ya wagombea wa nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa juni 29
mwaka huu.
Katibu mkuu wa kamati ya uchaguzi huo, Halid Kamguna
amesema mkutano huo utafanyika katika ukumbi wa Gymkan jijini Dar es saalam
majira ya saa 11:00 asubuhi.
Kamguna aliongeza kuwa jana kamati ya uchaguzi
ilikutana kumalizia zoezi la kuhakiki
fomu za wagombeo wote wa nafasi za uongozi, hivyo majina yote yataanikwa
kesho.
Moja ya wagombea waliokuwa kivutio kikubwa katika
nafasi za juu ni Evance Aveva na Michael Richard Wambura waliochukua fomu ya
kuwania Urais wa klabu hiyo.
Wagombea hawa waliteka hisia za wanachama wa klabu
ya Simba waliowasindikiza kwa mbwembwe nyingi wakati wa kuchukua na kurudisha
fomu.
Aveva na Wambura wanatarajiwa kuchuana vikali kwa
kuangalia jinsi walivyosindikizwa na watu wengi wanaoaminika kuwa wanachama wa
Simba.
Nafasi ya makamuwa rais,Jamhuri Kiwhelo `Julio`
alikuwa kivutio kikubwa, lakini wengine kama Geofrey Nyange Kaburu, na Joseph Itang`are
`Mzee Kinessi` walijitosa pia.
0 comments:
Post a Comment