Friday, May 2, 2014



Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

WAPENZI wa soka jijini Mbeya wanatarajia kuishuhudia timu yao ya taifa ya Tanzania, Taifa stars kwenye uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine mjini humo,  aprili 4 mwaka huu ikicheza na Malawi katika mechi ya kirafiki ya kimataifa.

Hii itakuwa mechi ya pili kwa Stars ya maboresho katika harakati zake za kujipima ubavu kabla ya kuanza kampeni za kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika, AFCON zitakazofanyika mwakani nchini Morocco.

Aprili 26 mwaka huu,  siku ya maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Taifa stars iliyosheheni wachezaji waliopatikana katika mpango wa maboresho ya Taifa stars ilicheza mechi ya kirafiki dhidi ya Burundi na kulala mabao 3-0.

Hii itakuwa ni mechi ya kwanza kwa kocha mpya wa Stars Mart Nooij kuiongoza Stars katika mechi ya kimataifa ya kirafiki.

Mechi ya kirafiki dhidi ya Burundi, kaimu kocha mkuu, Salum Madadi ndiye aliyekalia benchi , huku Nooij akiwa jukwaani kutazama vipaji.

Baada ya kuitazama Stars ikizama kwa Burundi, Mart Nooij aliongeza wachezaji tisa katika kikosi hicho

Wachezaji walioongezwa ni Edward Charles Manyama (JKT Ruvu), Elias Maguli (Ruvu Shooting), Hassan Dilunga (Yanga), Hussein Javu (Yanga), John Bocco (Azam), Kelvin Friday (Azam), Oscar Joshua (Yanga), Nadir Haroub (Yanga) na Shomari Kapombe (AC Cannes, Ufaransa).

Taarifa iliyotumwa na afisa habari wa TFF, Boniface Wambura Mgoyo kwa vyombo vya habari jioni hii inaelezwa kuwa timu ya Taifa ya Malawi (Flames) imewasili jijini Mbeya tayari kwa mechi ya kirafiki hiyo ya jumapili.

Wambura alisema Malawi imewasili jana (mei 1 mwaka huu) saa 1 jioni kwa njia ya barabara ikiwa na msafara wa watu 31 na imefikia hoteli ya Manyanya.

Nayo Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ipo jijini Mbeya tangu Aprili 27 mwaka huu kujiandaa kwa mechi hiyo.

Wambura ametaja Kiingilio katika mechi hiyo kuwa ni sh. 5,000 wakati tiketi zitauzwa siku ya mchezo kuanzia saa 2 asubuhi katika vituo vya Uyole, Mwanjelwa,, Mbalizi, Stendi Kuu, Holiday Inn na Uwanja wa Sokoine.

Magari yatakayoruhusiwa kuingia uwanjani ni ya wachezaji, gari la wagonjwa, gari la zimamoto na gari la waamuzi pekee.

Taifa Stars imepangiwa kucheza na Zimbabwe katika raundi ya pili ya mechi za mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika (AFCON) zitakazofanyika mwakani nchini Morocco.

Stars itaanzia nyumbani ambapo mechi ya kwanza itachezwa kati ya Mei 16 na 18 wakati ile ya marudiano itachezwa Harare kati ya Mei 30 na Juni 1 mwaka huu.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video