Monday, May 5, 2014



http://4.bp.blogspot.com/-PWURXV9SV6g/UGHLE0pJuFI/AAAAAAAAckI/s8wlPC89WXs/s1600/tn+(27).jpg
Na Braka Mpenja, Dar es salaam
CHAMA cha soka visiwani Zanzibar, ZFA kimebainisha kuwa ukosefu wa udhamini mnono kwenye michuano ya ligi kuu Zanzibar  kumeifanya isiwe na mvuto kama ilivyo kwa Tanzania bara.
Katibu mkuu wa ZFA, Masud Ettei ameuambia mtandao huu kuwa ligi kuu ya Zanzibar ina mdhamani mmoja tu ambaye ni Grand Malta, wakati huo huo klabu zinazoshiriki ligi hiyo hazina udhamini.
“Tunashukuru tunachokipata kwa mdhamini wetu, lakini anachotoa hakiwezi kukidhi mahitaji ya ZDF”
“Tungekuwa na udhamini mzuri tungekuwa bora kama ilivyo kwa Tanzania bara”.
“Unajua ZFA imetafuta mdhamini ambaye ni TBL chini ya kinywaji chake cha  Grand Malta, lakini timu zenyewe zimekosa udhamini kama vile Simba na Yanga ambazo mbali na wadhamini wa ligi Vodacom na  Azam TV , pia wana udhamini wa TBL”.
“Angalia Azam TV walivyoamua kuwekeza udhamini wao katika ligi, hii imeongeza chachu, hivyo nasisi Zanzibar tungetamani kuona udhamini kama huu”. Alisema Masud.
Masud ameomba makampuni mbalimbali kujitokeza kudhamini ligi ya Zanzibar pamoja na klabu zinazoshiriki ligi hiyi  ili iendane na kasi ya soka la kisasa.
“Klabu zikisaidiwa kwa udhamini, zitaweza kufanya maandalizi mazuri, zitalipa mishahara na posho kwa wachezaji kwa muda muafaka na kuinua hamasa”.
Aidha, Masud alisema Zanzibar ina wachezaji wazuri sana hasa vijana, lakini kukosekana kwa udhamini inawaumiza kichwa mno.
“Bara wenzetu wana michuano ya vijana kama Uhai Cup, lakini kwetu hakuna mashindano ya vijana. Tunao vijana wenye vipaji, lakini hatuna uwezo wa kuendesha mashindano”.
“Tunapendekeza makampuni yaje kutusaidia nasisi turudi katika kiwango cha juu kama ilivyo kwa wenzetu wa bara”. Aliongeza Masud.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video