Saturday, May 3, 2014



 10302029_722357961140073_1520041417937471076_n
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
MAKAMU mwenyekiti wa zamani wa Yanga sc, Bilionea, Davis Mosha ameushutumu uongozi wa sasa wa klabu hiyo kushindwa kuwabakiza wachezaji muhimu kikosini kuelekea msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara na michuano ya kimataifa.
Mosha ambaye ni mwanachama na shabiki mkubwa wa Yanga, ameshangazwa na uongozi wa klabu hiyo chini ya mwenyekiti Yusuf Manji kumwachia kiungo wake mkabaji, Frank Domayo na mshambuliaji Didier Kavumbagu  kwenda Azam fc.
“Tunajua Kavumbagu kaenda kule, labda ndiye walikuwa wanamhitaji”.
“Haya, tumekuja kusikia Domayo naye kaenda Azam, mara tunasikia fununu kuwa Mbuyu Twite naye anakwenda Azam”.
“Sasa ni nini kinaendelea hapa katikati, ni kwamba viongozi wanataka kuondoka na kuacha timu haina wachezaji kwasababu wamesema hawagombei tena au wanataka kuleta wachezaji wazuri zaidi kuliko hao”. Alisema Mosha kwa masikitiko makubwa.
 FRANK DOMAYO
“Yanga iliyoanzishwa mwaka 1934 haina uwanja. Timu ya Azam iliyoanzishwa juzi ina uwanja, timu ya Azam ina TV, timu ya Azam imekuja juzi sasa inachukua wachezaji Yanga. Hii ni aibu, sisi ndio tunatakiwa kuchukua wachezaji Azam”.
“Itafika mahali tutabaki tuna historia ya wanachama nchi nzima, lakini hatuna maendeleo yoyote. Kama Azam wanachukua wachezaji wetu manake itafika wakati na wanachama watahamia Azam”.
Akizungumzia kuhusu kuwa kiongozi wa Yanga kwa mara nyingine, Mosha alisema hana kinyongo kuwa kiongozi wa klabu hiyo kwasababu yeye sio kiongozi, lakini bado wanamfuata na hilo ndilo jambo la msingi zaidi.
“Sio unaonekana kiongozi halafu hauisaidii Yanga. Mimi nina mapenzi na Yanga, sijawa na mapenzi na yanga jana au leo, nimekuwa na mapenzi na Yanga miaka mingi”.
“Na ndio maana wana Yanga wengi wananikubali, mambo ya Yanga mimi nabishana mpaka mwisho, nabishana mpaka kufa kuhusu Yanga. Siwezi kusema labda kwasababu nyie waandishi mnaniuliza”.
“Devis Moshi ni Yanga na nitaendelea kuisaidia Yanga. Si kwasababu ya kipato nilichonacho, hata kabla ya kipato”.
“ Kama unakumbuka historia ya nyuma, mimi nimekuwa nikiisapoti Yanga tangu nikiwa timu ya Ushirika ya Moshi”.
10297555_745886905451668_4947273067470024067_n
Aidha, Mosha amewataka wanachama kuwa makini kuelekea uchaguzi ujao utakaofanyika mwezi juni mwaka huu ili wasichague bora kiongozi kwasababu wamejifunza.
Alisema wasimchague mtu kwasababu labda sura yake ni nzuri na amejipaka mafuta wakaona anafaa, bali waangalie watu wenye historia na mapenzi ya Yanga.
“Tumechukua watu wasiojulikana, hatimaye Yanga yetu inakufa”.
“Mimi nilitoka kwenye uongozi baada ya kuona nina watu wasioipenda Yanga, nikaona nisije kuchafua jina langu”.
“Ushauri wangu ni kwamba kiongozi anayekuja Yanga awe ni Yanga na awe anaipenda Yanga na awe anatoa muda wake mwingi kuisaidia Yanga”.
“Usitake kuwa kiongozi kwa kutaka jina, awe kiongozi kwa kuonesha mapenzi yake na nia yake ya kuisaidia timu. Asije akachukua uongozi halafu kesho akaona unamkera na kuamua kufanya mambo yake”. Aliongeza Mosha.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video