Wednesday, May 7, 2014



Staz
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
MCHAKATO wa maboresho ya timu ya taifa ya Tanzania, Taifa stars uliohusisha makocha mbalimbali kuzunguka mikoani kwa lengo la kung`amua vipaji vilivyofichika  umeendelea kukosolewa na baadhi ya wataalamu wa soka.
Akizungumza na mtandao huu, kocha msaidizi wa Mbeya City fc,  Maka Mwalwisyi amesikitishwa sana na shirikisho la soka Tanzania TFF, kuamua kutumia mfumo huu badala ya kuhangaika kujenga msingi wa soka ambao ndio kilio cha watanzania wengi.
Maka alisema watanzania kwasasa hawahitaji kuona TFF inahangaika na timu ya Taifa kwa kutafuta wachezaji wasiocheza ligi kuu, kwasababu kupata mafanikio kwa mfumo wa sasa ni ngumu sana na hata mataifa makubwa hayawezi kutengeneza timu ya taifa inayojiandaa na mashindanio mwaka mmoja mbele kwa mfumo huu.
“Mimi nashangaa sana na nitaendelea kushangaa, kwanini makocha walipitisha mpango huu?, hivi kama kweli mchezaji yupo Mbeya na ana kiwango cha juu, sisi Mbeya City tutashindwa kumuona kweli? Hata wenzetu Prisons wasimuone, hapana”.
‘Wanachagua makocha kuzunguka nchi nzima na kutumia fedha nyingi, sidhani kama ni suluhisho, kuna mambo mengi ya kuyafanya hasa kujenga misingi ya soka la vijana”.
“Mchezajai hachezi ligi, unamchukua kutoka mchangani na kumleta Taifa stars, halafu unawadanganya watanzania kuwa unataka uipeleke timu AFCON mwakani nchini Morocco”.
‘Hivi huyu mchezaji ambaye hachezi ligi, itakuwaje akikutana na wachezaji wanaoshindia mpira kama magharibi mwa Afrika?, hivi ni vichekesho tu”. Alisema Maka.
Kocha huyo aliongeza kuwa TFF wangeshauriwa kuendeleza timu ya `Young Future Taifa stars` iliyoanzishwa na kocha aliyevunjiwa mkataba, Mdenish Kim Poulsen kwasababu ilijumuisha wachezaji wa ligi kuu.
“Kim alikuja na mpango mzuri, lakini wameona kama haufai”.
“ Ile timu ya Young Future Taifa stars ndio ingewekwa kambini miezi miwili Tukuyu, angalau tungepata watu fulani”
“ Lakini kwa kikosi chao kile cha maboresho, hawajafanya kitu pale na nashukuru watanzania kugundua hilo kwasababu nawasikia wakisema”.
“Nadhani kocha Mart Nooij aliwaambia kuhusu wachezaji hawa. Niliwaona na kugundua kuwa hawana msaada kwa Stars. Ndio maana hawakupangwa hata kwenye mechi dhidi ya Malawi”.
“Rais Malinzi na watu wake wakae chini tena kuufikiria mfumo huu. Nadhani si busara kuacha kila lililokuwa linafanywa na watu wa nyuma”.
“Mazuri yaendelezwe na mabaya yasahihishwe , lakini kwa mwendo huu nakuw a na mashaka”.
‘Unashindwa kuchukua wachezaji kutoka Mbeya City fc iliyomaliza nafasi ya tatu”
“ Unakwenda kutafuta watu wasiojulikana kwa kutumia fedha nyingi na hawachezi ligi, hakika unaleta utani tu”. Alimaliza Maka.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video