Wednesday, May 7, 2014

In action: Goalscorer Joe Allen (left) tries to win the ball from Palace striker Marouane Chamakh
Kazini: Mfungaji wa bao la kwanza la Liverpool jumatatu ya wiki hii, Joe Allen (kushoto) akichuana na mshambuliaji wa Palace,  Marouane Chamakh
Amazing: Gayle celebrates with Yannick Bolasie, sparking roaring scenes at Selhurst Park
Ajabu: Gayle akishangilia na Yannick Bolasie, baada ya kuchafua hali ya hewa kwa Liverpool uwanja wa Selhurst Park

No avail: Palace keeper Julian Speroni can't stretch to stop Daniel Sturridge's goal for Liverpool's second
Manyoya tu: Kipa wa Palace, Julian Speroni akishindwa kuokoa mpira uliopigwa na Daniel Sturridge na kuifungia Liverpool bao la pili.
Iconic: Suarez celebrates match Alan Shearer and Cristiano Ronaldo's record of 31 goals in a season
Suarez akishangilia kufikia rekodi ya Alan Shearer na Cristiano Ronaldo ya mabao 31 kwa msimu mmoja, lakini timu yake ilitoka sare ya 3-3 na kumwaga machozi baadaye.
Rodgers refuses to give up on Liverpool title win
Brendan Rodgers

KOCHA Liverpool, Brendan Rodgers bado hajakata tamaa ya kutwaa ubingwa wa ligi kuu soka nchini England licha ya kuharibiwa na Crystal Palace jumatatu ya wiki.

Mabao ya Damien Delaney  na  Dwight Gayle  katika dakika 11 za mwisho yalipunguza kasi ya Liverpool na kutoka sare ya 3-3, hivyo kuwafanya Manchester City wawe na asilimia kubwa zaidi ya kutwaa ubingwa.

Rodgers ambaye timu yake ipo kileleni kwa pointi moja mbele lakini wakiwa na mchezo mmoja zaidi ya Man City alisema Liverpool itaendelea kupigana mpaka mwisho wa msimu, licha ya wengi kuamini mbio za ubingwa ziliisha jumatatu.

“Wachezaji bado wapo katika morali na wamewaomba mashabiki wao kutofuta ndoto za ubingwa”. Alisema.

“Kuwa na timu ambayo ipo mbele kileleni kwa pointi moja huku tukiwa na wiki moja ya kwenda ni jambo zuri”

“Huwezi kujua nini kitatokea, sisi tutajituma mpaka mwisho”.

“Ninachoweza kuahidi ni kuwa, kwa vile nipo hapa, timu itapigana kufa na kupona. Msimu haujaisha mpaka mechi yetu na Newcastle”.

Rodgers amewashukuru wamiliki wa timu kwa kuwa na imani kubwa na yeye na kuna taarifa kuwa atapewa mkataba mpya.

“Napenda kuwashukuru wamiliki na mkurugenzi wa timu kwa kile wanachonifanyia tangu nimefika hapa.” Rodgers alisema.

“Walimleta kocha kijana mwenye miaka 39 katika moja ya klabu kubwa duniani na kunipa nafasi ya kujiendeleza katika falsafa yangu ya mpira”.

“Kama sio imani yao kwangu, yawezekana nisingekuwepo hapa ukizingatia uhalisia wa soka la kisasa”.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video