MSHAMBULIAJI wa Atletico Madrid, Diego Costa, ameitandika Chelsea bila huruma na kuisaidia klabu yake kufuzu
fainali licha ya kuwepo kwa tetesi kuwa atajiunga na Chelsea majira ya kiangazi
mwaka huu.
Costa alifunga bao la penati na katika ushindi wa
mabao 3-1 dhidi ya Chelsea na kumfanya Diego Simeone akutane na Carlo Ancelotti
katika mchezo wa fainali mjini Lisbon nchini Ureno mwezi ujao.
Mtandao huu kupita mtandao rafiki wa Goal.com unafahamu kuwa Chelsea
wametenga kitita cha pauni milioni 35 kukamilisha usajili wa nyota huyo mwenye
miaka 25.
Costa amekiri kuwa kwasasa hajaamua maisha yake ya
baadaye.
“Kucheza Chelsea baadaye? Tutaona, najua kuna ofa
kwa ajili yangu, najisikia vizuri kuwepo Atletico” ameuambia mtandao wa Sky Italy.
Adrian Lopez na Arda Turan pia walifunga, lakini
Chelsea walikuwa wa kwanza kufumania nyavu za Atletico kupitia Fernando Torres.
Costa ameuelezea mchezo wa leo kuwa ni “wa maajabu
na historia” na amemsifu kocha wake Diego Simeone kuifanya Atletico kuwa na
makali zaidi msimu huu.
“Ni kitu cha ajabu na kihistoria. Tumejituma kwa
nguvu zote kufika fainali hii”. Costa amezungumza na Canal Plus.
“Mpira haukuishia kwenye penati tu, lakini
ulimalizika vizuri. Nadhani timu inafanya vitu sahihi, lakini Diego Simeone
amefanikiwa kufanya maamuzi sahihi kila wakati”.
0 comments:
Post a Comment