Msanii Lucas Mhavile maarufu kwa jina la ‘Joti’ baada ya kukaa kimya kwa mda sasa ameibuka na filamu yake ya Joti Sanduku la Babu ambayo amecheza katika husika tofauti tofauti filamu hiyo itakuwa ikisambazwa na Kampuni ya proin promotions ya jinini Dar es salaam
Akizungumzia filamu hiyo Joti alisema kuwa amekuja kivingine kwani kitu alichofanya katika filamu hiyo haijawahi kutokea wala kufanywa na mtu yoyote yule katika tasnia hii ya filamu nchini.
Hivyo wapenzi wake wakae mkao wa kula kwani wakati wowote kuanzia sasa itakuwa inaingia sokoni.
Filamu hii si yakukosa maana unaambiwa uzee mwisho chalinze mjini kila mtu `honey`.
Joti amewaomba wapenzi wa filamu kununue nakala halisi pindi itakapotoka.
Katika filamu hii, Joti ameelezea mambo mbalimbali ya ujana, usichana pamoja na uzee
Mbali na hivyo, filamu hiyo imebeba mambo matatu muhimu kwanza ina burudisha, pia ina elimisha na kupata ujumbe muhimu kabisa katika jamii inayotuzunguka’
Filamu hiyo ya kwanza tangu Joti aweke kando mambo ya filamu na kujiingiza katika mambo ya uchekeshaji kupitia luninga sasa amerudi tena katika filamu
yake mwenyewe inayokwenda
0 comments:
Post a Comment