Wednesday, May 7, 2014



 Jerry Santo in action
KIUNGO wa Coastal Union, Mkenya Jerry Santo anataka kurudi Simba sc msimu ujao wa ligi kuu soka Tanzania bara, mtandao wa Goal.com umeandika.
Santo kwa sasa ni mchezaji huru baada ya mkataba wake wa miaka miwili katika klabu ya Coastal Union kumalizika msimu huu.
Kiungo huyo siku za nyuma aliichezea Simba baada ya kujiunga nayo kutokea Tusker ya Kenya mwaka 2009.
Santo alishinda taji la Kenya akiwa na Tusker mwaka 2006 na mwaka 2009 aliteuliwa kuwa nahodha katika misimu yake mitatu klabuni hapo.
Santo ameuambia mtandao wa Goal.com kuwa hayuko tayari kuongeza mkataba na Coastal,  kwasababu hana furaha na mazingira ya timu hiyo iliyomaliza msimu katika nafasi ya 8.
“Mazingira yaa Coastal Union sio mazuri kwa upande wangu, lakini sasa nataka kurudi Simba ambako nilicheza kwa mafanikio makubwa na kurudi timu yangu ya Taifa, `Harambee Stars`, alisema Santo katika mahojiano maalum na Goal.com

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video