Anaondoka? James Milner amewaambia Manchester City kuwa anataka kuondoka.
JAMES Milner anataka kuondoka Manchester City, huku Arsenal wakionesha nia ya kutaka kumsajili majira ya kiangazi mwaka huu.
Nyota
huyo mwenye miaka 28 amechoka kukosa namba ya kudumu na amemwambia
kocha mkuu Manuel Pellegiri kuwa anataka kuondoka kutafuta maisha
mengine.
Taarifa
hizo ni njema kwa Aserne Wenger ambaye yuko katika harakati za kujenga
kikosi cha ushindani msimu ujao kwa lengo la kusaka ubingwa wa ligi kuu
soka nchini England.
Arsene Wenger yuko makini kufautailia dili hili na yuko tayari kuweka ofa ya pauni milino 10 kwa nyota huyo wa kimataifa ya England.
Micah
Richards, Jack Rodwell, Scott Sinclair, Gareth Barry na Joleon Lescott
wote wanatarajiwa kuondoka Etihad.
Kama itatokea hivyo, mlinda mlango Joe Hart ndiye atabaki mchezaji pekee wa Kiingereza katika klabu hiyo, japokuwa Gael Clichy na Dedryck Boyata nao wana vigezo.
Kama Milner, na wachezaji wengine wataondoka, basi Joe Hart atabaki mchezaji pekee wa Kiingereza katika klabu ya Man City
0 comments:
Post a Comment