MSHAMBULIAJI wa Manchester United, Mholanzi, Robin
Van Persie anaweza kuanzia benchi katika mchezo wa ligi kuu nchini England
dhidi ya Sunderland jamamosi ya wiki hii.
Mholanzi huyo hajapangwa kutokana na majeruhi ya
goti tangu Alipopiga Hat-Trick dhidi ya Olympiakos hatua ya 16 ya UEFA na
kuiwezesha timu kufuzu robo fainali machi 19 mwaka huu.
RVP alirejea katika mazoezi ya ya Mashetani wekundu uwanja wa Carrington
ijumaa ya wiki iliyopita na tangu hapo amekuwa akiendelea vizuri, na kuongeza
matumaini ya kuwavaa vijana wa Gus Poyet wikiendi hii.
Awali nyota huyo alikuwa anatarajiwa kukosa mechi
zote zilizosalia za msimu huu na ushiriki wake katika fainali za kombe la dunia
majira ya kiangazi mwaka huu kuwa katika wasiwasi, lakini kurudi mapema
kumeongeza nguvu kwa Man United na timu ya Taifa ya Uholanzi.
Kocha wake wa timu ya taifa, Louis Van Gaal ambaye
anatarajiwa kutangazwa kuwa kocha wa Man United muda wowote amemuongezea nguvu
zaidi.
Wawili hao wanamtumia wakala mmoja, bwana Kees Vos
na wapo katika mahusiano mazuri.
0 comments:
Post a Comment