Thursday, May 1, 2014



MSHAMBULIAJI wa Manchester United, Mholanzi, Robin Van Persie anaweza kuanzia benchi katika mchezo wa ligi kuu nchini England dhidi ya Sunderland jamamosi ya wiki hii.
Mholanzi huyo hajapangwa kutokana na majeruhi ya goti tangu Alipopiga Hat-Trick dhidi ya Olympiakos hatua ya 16 ya UEFA na kuiwezesha timu kufuzu robo fainali machi 19 mwaka huu.
RVP alirejea katika mazoezi ya  ya Mashetani wekundu uwanja wa Carrington ijumaa ya wiki iliyopita na tangu hapo amekuwa akiendelea vizuri, na kuongeza matumaini ya kuwavaa vijana wa Gus Poyet wikiendi hii.
Awali nyota huyo alikuwa anatarajiwa kukosa mechi zote zilizosalia za msimu huu na ushiriki wake katika fainali za kombe la dunia majira ya kiangazi mwaka huu kuwa katika wasiwasi, lakini kurudi mapema kumeongeza nguvu kwa Man United na timu ya Taifa ya Uholanzi.
Kocha wake wa timu ya taifa, Louis Van Gaal ambaye anatarajiwa kutangazwa kuwa kocha wa Man United muda wowote amemuongezea nguvu zaidi.
Wawili hao wanamtumia wakala mmoja, bwana Kees Vos na wapo katika mahusiano mazuri.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video