PEP
Guardiola amekiri kuwa haikuwa kazi nyepesi kurithi mikoba ya Jupp Heynckes
katika klabu ya Bayern Munich msimu huu baada ya kocha huyo kushinda makombe
matatu ikiwemo la nyumbani na Ulaya.
Guardiola
aliwashuhudia vijana wake wakiifunga Borussia Dortmund mabao 2-0 na kubeba
kombe la DFB-Pokal siku ya jumamosi.
Mbali
na kombe hilo, kocha huyo pia alitwaa ubingwa wa Bundesliga katika msimu wake
huu wa kwanza klabuni hapo.
Hata
hivyo mafanikio hayo yamezibwa na kufanya vibaya katika michuano ya UEFA ambapo
walitolewa hatua ya nusu fainali kwa kipigo cha mbwa mwizi dhidi ya Real
Madrid.
“Ni
mwaka wangu wa tano nikiwa mkufunzi wa soka , mwaka wangu wa sita nikiwa kocha
mkuu”. Guardiola aliwaambia waandishi wa habari.
“Mwaka
mmoja nilikuwa naifundisha Barcelona B. Baada ya miaka minne nilikuwa kocha
mkuu wa Barcelona. Kipindi hiki kilikuwa muhimu kwangu na nilikabiliana na
changamoto nyingi katika maisha yangu ya ukocha”.
“Hapa
Ujerumani sijafanikiwa na ndio maana kila wakati nawahamasisha wachezaji wangu.
Baada ya Bayern kushinda mataji matatu chini ya Jupp Heynckes, haikuwa rahisi
kwangu”.
“Bado
sijafanikiwa kuiweka timu nipendavyo mimi. Kuna kazi kubwa ya kufanya, lakini
tunajivunia kwa makombe haya”.
Pia
Guardiola ameisifu bodi ya Bayern kwa kumpa kibarua na kusema anataka kuwaletea
mafanikio zaidi.
0 comments:
Post a Comment