Thursday, May 8, 2014



Giggs to tell Van Gaal - 'I'm ready to play on'
RYAN Giggs anatarajia kumwambia kocha anayekuja kujiunga na Manchester United,  Louis Van Gaal kuwa anahitaji kuendelea kucheza na kumalizia soka lake Old Trafford kwa msimu mwingine.

Giggs aliyepewa mikoba ya ukocha mkuu Man United baada ya David Moyes kutimuliwa mwezi uliopita, alicheza dakika 20 za mwisho katika ushindi wa 3-1 dhidi ya Hull City jumanne usiku, huku wengi wakiamini kuwa mechi hiyo ilikuwa ya mwisho kwake kucheza Old Trafford.

Lakini mkongwe huyo mwenye miaka 40 bado anajiona kuwa na nguvu za kuendelea kushiriki mikikimikiki ya ligi kuu nchini  England na taarifa kutoka Carrington zinasema kuwa hakuna sababu ya Giggs kutoendelea kucheza na kuifundisha klabu hiyo kwa msimu ujao.

Van Gaal anatarajiwa kutangazwa kuwa kocha wa United wiki ijayo na hatima ya baadaye ya Giggs haijulikani kwani mpaka sasa Mholanzi huyo hajataja majina ya watakaokuwa wasaidizi wake.

United wamepokea vizuri mwanzo wa Giggs klabuni hapo, lakini maamuzi ya mwisho juu ya kocha huyo mchezaji kuendelea kuwepo benchi la ufundi msimu ujao yapo juu ya Van Gaal.

Kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Uholanzi, Patrick Kluivert hatajumuika na Van Gaal Old Trafford na hii inatoa nafasi kubwa kwa Giggs kupewa ofa ya kuwa kocha msaidizi.

Tangu apewe ukocha mkuu wa muda kurithi mikoba ya Moyes, Giggs ameiongoza Man United kushinda mechi mbili Old Trafford dhidi ya Nowrich City na Hull City, lakin aliachwa mdomo wazi baada ya kufungwa bao 1-0 na Sunderland.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video