Thursday, May 8, 2014



 http://api.ning.com/files/VMB94olbxS1KUXphY0U47D4laBLxC*CFhUlgLRS9F0nyaxUKrUNPfsr0M0JTm2GFIFYUVc9GC7kbzapFvqrS-DcuQ0M-I6aJ/PLUIJMKITAMBI.jpg?width=650
TAARIFA za uhakika zilizoufikia mtandao huu dakika chache zilizopita ni kwamba kocha mkuu wa Young Africans, Mholanzi, Hans Van der Pluijm amepata kazi mpya nchini Saudi Arabia.
Pluijm aliyejiunga na Yanga mapema januari mwaka huu umepata shavu hilo katika klabu ya Al Shoalah FC inayoshiriki ligi kuu soka nchini humo.
Kocha huyo anaondoka baada ya kushindwa kutetea ubingwa na kuzidiwa kete na kocha wa Azam fc Joseph Marius Omog msimu huu ambao Yanga walimaliza katika nafasi ya pili.
Pluijm alirithi mikoba ya mholanzi mwenzake, Ernie Brandts aliyetimuliwa mwezi desemba mwaka jana baada ya kufungwa mabao 3-1 na Simba sc katika mechi ya Nani Mtani Jembe.
Hata hivyo, Pluijm alikuwa na mtababa mfupi wa miezi sita na Yanga ambao unatarajia kumalizika mwezi ujao.
Sasa Yanga wanaingia katika kibarua kingine cha kusaka kocha mkuu atakayesaidiana na kocha msaidizi Charles Boniface Mkwasa.
Mtandao huu unaendelea kufuatilia taarifa hii na baadaye utapewa habari nzima. Tafadhali endelea kuwa nasi.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video