Tuesday, May 6, 2014



 http://e2.365dm.com/13/09/800x600/nemanja-vidic-manchester-united_3002191.jpg?20140109095214
BEKI wa kushoto wa Manchester United, Mfaransa Patrice Evra amesema itawauma sana pale nahodha wao, Nemanja Vidic atakapoondoka klabuni hapo na kujiunga na Inter Milan majira ya kiangazi mwaka huu.
Uhamisho wa Vidic kwenda Italia ulithibitishwa mwezi machi mwaka huu baada ya nyota huyo kugoma kuongeza mkataba Man United.
Mserbia huyo akiwa na United ameshsinda makombe matano ya ligi kuu na UEFA mwaka 2008.
Evra ambaye anaweza kujiunga na mserbia huyo katika klabu ya Inter majira ya kiangazi, amecheza kwa muda mrefu na Vidic tangu wote kwa pamoja wajiunge na Manchester United wakati wa dirisha dogo la usajili mwaka 2006.
Mfaransa huyo naye anamaliza mkataba wake majira ya kiangazi mwaka huu na bado anapima hatima ya namba yake msimu ujao ili kuamua kubaki au kuondoka.
“Inauma sana kumpoteza Vida.” Mfaransa huyo ameiambia tovuti ya United. “Kwa mimi, ni beki bora zaidi wa kati. Unapoona mchezaji kama Vidic anaondoka klabuni, inahuzunisha sana”.
“Unapozungumzia Vida, kama unanizungumzia mimi. Tulijiunga na klabu pamoja. Nakumbuka mechi ya kwanza ilikuwa ngumu sana. Katika mechi moja wote tulikuwa wachezaji wa akiba. Tulikuwa na kiwango cha chini.
“Rene Meulensteen alikuwa kocha wa wachezaji wa akiba na alituchukua wote. Tulikuwa tunazungumza kwenye vyumba vya kuvalia nguo: “ Oh mwanangu, kwanini tumekuja Manchester?, tungebaki katika klabu zetu za zamani”.
“Ilikuwa wakati mgumu sana, lakini tuliimarika kwa pamoja. Tulikuwa tunalala hoteli moja na kwenda mazoezini pamoja, tulishinda mataji pamoja. Kiukweli nahuzunika sana kumpoteza”.  Alisema Evra.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video