BRENDAN
Rodgers bado anasubiria mshambuliaji wake Daniel Sturridge awe fiti tayari kwa safari
ya kuwafuata Crystal Palace katika mchezo muhimu wa ligi kuu nchini England
siku ya jumatatu wiki ijayo.
Mshambuliaji
huyo wa kimataifa wa England alitolewa nje katika ushindi wa 3-2 dhidi ya
Manchester city, aprili 13 mwaka huu kutokana na majeruhi ya nyama za paja na wiki
iliyofuata alikosa mechi dhidi ya Nowrich
ambayo Liverpool walishinda mabao 3-2.
Sturridge
alianzia benchi na kuungizwa baadaye katika mechi ya jumamosi iliyopita dhidi
ya Chelsea na kushuhudia klabu yake ikilala mabao 2-0 na kuwa hatarini kukosa
ubingwa ambao hawajabeba kwa miaka 24 sasa.
Katika
mkutano wa jana jioni na waandishi wa habari, Rodgers alikiri kuwa mechi na
Chelsea nyota wake hakutakiwa kucheza na kuelekea mchezo muhimu wa jumatatu
kwenye uwanja wa Selhurst Park wanasubiria kuimarika kwake.
“Tutaangalia
ndani ya saa 48 zijazo. Hajafanya mazoezi tangu alipopata majeruhi, kidogo
ilikuwa kazi ngumu kwake dhidi ya Chelsea”. Rodgers aliwaambia waandishi wa
habari.
“Tulifanya
jitihada kubwa ili kumrudisha na tulihitaji awepo hata benchi, lakini kwa
bahati mbaya haikutusaidia”.
“Anapokuwa
katika hali nzuri anafanya kazi kubwa. Amekuwa karibu zaidi na madaktari wa
klabu wiki hii. Ataungana na wenzake, lakini tutaona jinsi itakavyokuwa jumatatu”.
Aliongeza Rodgers.
Mshambuliaji
mwenzake na Sturridge, Luis Suarez alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwaka wa
PFA nchini England jumapili iliyopita baada ya kufunga mabao 30 katika mechi 31
za ligi kuu.
Rodgers
alikiri kuwa mshambuliaji wake huyo raia wa Uruguay alipambana sana na kustahili
tuzo hiyo kwasababu kwa wakati wote amekuwa katika kiwango cha juu.
“Hongera
zake. Ilikuwa zawadi iliyotokana na jasho lake”, Aliongeza kocha huyo wa zamani
wa Swansea City.
“Amekuwa
na kiwango kikubwa katika klabu msimu huu”.
“Kwahiyo
alistahili na najua ana heshimu sana tuzo hiyo, kutokea miongoni mwa wachezaji
wengi wa nchi hii si kazi nyepesi. Najua ana furaha”.
0 comments:
Post a Comment