Saturday, May 10, 2014



 Cruyff: Atletico Madrid deserve to win La Liga
GWIJI  wa soka FC Barcelona, Johan Cruyff amesema Atletico Madrid wanastahili kushinda taji la La Liga msimu huu.
Cruyff na Hristo Stoichkov walipewa nafasi ya kutabiri timu gani itachukua ubingwa, lakini Crufy ameinyima nafasi timu yake ya zamani ya Barcelona na Real Madrid.
Kwasasa Atletico wapo mbele kwa pointi tatu dhidi ya Barca ambao watacheza nao mechi ya kufunga msimu.
Cruyff anaamini vijana wa Diego Simeone watakaokutana na wapinzani wao wa mji katika fainali ya UEFA, wana nafasi ya kuchukua `ndoo` na hata kama watakosa bado wanatakiwa kupongezwa kwa kuonesha kiwango cha juu msimu huu.
“Atletico wanastahili kutwaa ubingwa na kama itatokea wamekosa,  watajipanga kwa msimu ujao”. Aliwaambia waandishi wa habari.
Wakati huo huo itakuwa mbaya zaidi kwa Barcelona kama watakosa ubingwa baada ya kutolewa na Atletico katika michuano ya UEFA hatua ya nusu fainali.
Pia walipoteza mchezo wa fainali wa kombe la mfalme ` Cope del Rey ` dhidi ya Real Madrid,na nyota huyo wa zamani wa Barca alisema matokeo hayo ni udhaifu wa bodi isiyoelewa mpira.
“Maamuzi yanachukuliwa na watu wa juu na kufanya yawe magumu kutekelezeka, kwasabau watu wa juu hawajui mpira”. Alisema.
“Siku zote kama unajua mpira, utagundua kwanini mlifanya vizuri na sasa mnafanya vibaya”.
Nyota huyo wa zamani aliongeza: “sidhani kama Real Madrid watashinda mataji yote matatu msimu huu”.
Kwa upande wake Stoichkov alitabiri kuwa wakatalunya watabeba taji la Las Liga, huku Atletico Madrid wikiifunga Real Madrid kwenye fainali ya UEFA.
“Inanikumbusha wakati Deportivo walipopoteza Riazor (1992). Tulitegemea Deportivo hawashindi,  na kwa mfano huu, Barca watakuwa mabingwa kama watashinda mechi zao mbili”.
“Lolote linaweza kutokea, hii ni kweli; lakini Barca watashinda La Liga na Atletico watashinda UEFA.”
“Madrid wana Copa del Rey. Hawana ubavu tena, na walidhani wangeshinda makombe matatu, lakini hilo haliwezi kutokea”.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video