Sunday, May 4, 2014


 Doubt: Eden Hazard was fouled in the Norwich box but the referee blew for offside

CHELSEA imeshindwa kupanda kileleni katika msimamo wa ligi kuu soka nchini England baada ya kutoka suluhu pacha ya bila kufungana na Nowrich City.
Kwa matokeo ya leo, Mourinho anabakia katika nafasi ya tatu akiwa na pointi 79 baada ya kucheza mechi 37.
Kama Chelsea wangeshinda leo wangefikisha pointi 81 kileleni, huku wakisubiri matokoe ya mechi ya kesho kati ya Liverpool dhidi ya Crystal Palace.
Ili kutwaa ubingwa, Chelsea wanasubiri maajabu ya soka kutokea kwasababu wanaomba Man City na Liverpool wapoteze mechi zao zote za mwisho na wao kushinda mechi yao.
 Disbelief: John Terry reacts to Neil Swarbrick's decision to blow his whistle for offside
Kama Liverpool na Man City watapoteza mechi zote, halafa Mourinho akashinda basi atakaa kileleni kwa pointi 82.
Lakini kwa kiwango cha Man City na Liverpool kupoteza mechi zote yatakuwa ni maajabu makubwa katika ulimwengu wa soka.
Man city wapo kileleni kwa pointi 80 kufuatia ushindi wa mabao 3-2 waliopata jana dhidi ya Everton katika dimba la Goodison Park.
Liverpool wapo nafasi ya pili kwa pointi 80, lakini wanazidiwa wastani wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Ili kutwaa ubingwa, Liverpool waliocheza mechi 36 sawa na Man City wanahitaji kushinda mechi zote mbili huku wakiombea Man City ashinde mechi moja na kutoa sare moja.
Kama Man City na Liverpool watashinda mechi zao zote za mwisho, bingwa atapatikana na kwa wastani wa mabao ya kufunga na kufungwa, lakini Man City watakuwa wapo sehemu nzuri.
Mpaka sasa, Liverpool wamefunga mabao 96 na kufungwa mabao 46, ukitoa mabao ya kufunga na kufungwa unapata mabao +50.
Man City wamefunga mabao 96 na kufungwa 37, ukitoa mabao ya kufunga na kufungwa unapata +59.
Kwa hesabu hizo, Liverpool atahitaji kushinda mechi zake zote kwa mabao mengi zaidi ili kufuta tofauti ya mabao 9.
 article-2620048-1D9180BF00000578-38_634x361
Katika mechi nyingine, bao pekee la Mfaransa Olvier Giroud limewapa ushindi wa bao 1-0 Arsenal dhidi ya West Ham.
Kwa matokeo hayo, Asernal wamejihakikisha kumaliza nafasi ya nne na kufuzu UEFA mwakani.

BAADA YA MECHI ZA LEO HUU HAPA MSIMAMO WA EPL

English Barclays Premier League | LOGS

PosTeamPWDLGFGAGDPts
1Manchester City36255696375980
2Liverpool36255696465080
3Chelsea37247669264379
4Arsenal37237766412576
5Everton37209859392069
6Tottenham Hotspur37206115251166
7Manchester United361861260411960
8Southampton371510125345855
9Newcastle United37154184257-1549
10Stoke City371211144351-847
11Crystal Palace36134192843-1543
12West Ham United37117194049-940
13Swansea City37109185153-239
14Aston Villa36108183954-1538
15Hull City36107193748-1137
16West Bromwich Albion36715144255-1336
17Sunderland3698193857-1935
18Norwich City3789202860-3233
19Fulham3794243883-4531
20Cardiff City3779213172-4130

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video