Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
MSHAMBULIAJI wa zamani wa Yanga SC, Tukuyu Stars na timu ya taifa ya Tanzania, Taifa stars,
Seklojo Johnson Chambua amewapongeza Azam fc kwa usajili wanaoendelea kuufanya
ili kuimarisha kikosi chao kwa ajili ya mashindano ya kimataifa.
Chambua amesema usajili huo ni jambo lenye sura
mbili tofauti ambapo upande wa kwanza ni kwa Yanga na wa pili kwa Azam fc.
“Kwa mashabiki wa Yanga wameumia kwasababu
wameondokewa na wachezaji wao, lakini kwa upande wa Azam wamefurahi kwasababu
wameimarisha kikosi chao”.
“Azam watakuwa wanaiwakilishi nchi katika michuano
ya klabu bingwa Afrika mwakani, kwahiyo wapo katika kuimarisha kikosi chao”.
Salum Abubakar `Sure Boy ataungana na Frank Domayo kurekebisha mambo safu ya kiungo ya Azam fc |
“Taswira ya Azam kusajili si kuikomoa timu yoyote
bali ni kuimarisha kikosi chao. Inawezekana wanasajili kuimarisha kikosi na
siamini kama wanawakomoa Yanga”.
“Nadhani Yanga nao wanahitaji kujipanda kwa ajili
ya kombe la shirikisho, lakini kwa wachezaji hawa kuondoka inawezekana ni
matakwa yao binafsi”. Alisema Chambua.
Akizungumzia jinsi Domayo atakavyosuka kiungo cha
Azam na Salum Abubakar `Sure Boy`, Sekloja alisema wachezaji hawa wanafahamiana
kwasababu wamecheza timu ya Taifa kwa muda mrefu hivyo watakuwa msaada mkubwa
kwa klabu yao.
“Sure boy na Domayo japokuwa walikuwa wanacheza
timu tofauti, lakini wamekutana mara nyingi timu ya taifa. Nadhani itakuwa
rahisi kwa kocha Omog kuwachezesha pamoja”. Aliongeza Seklojo.
0 comments:
Post a Comment