Daniel Sturridge akila bata wiki hii na mpenzi wake kwenye fukwe za Miami .
MSHAMBULIAJI
wa Liverpool, Daniel Sturridge wiki hii anakula bata na mpenzi wake
mjini Miami kabla ya kujiunga na kikosi cha timu ya taifa ya England kwa
ajili ya kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil.
Nyota huyo wa majogoo wa jiji alitajwa katika kikosi cha wachezaji 23 cha Roy Hodgson.
Sturridge
mwenye miaka 24 katika kipindi hiki cha mapumziko amechagua kwenda
Florida- licha ya England kuwa na mpango wa kwenda Miami kucheza mechi
mbili za kirafiki.
Hodgson aliweka wazi kuwa hataki kuona wachezaji wake wanasafiri kwenda mbali kabla ya mashindano kuanza.
"Kam sijasahau, nitawasimamia wachezaji kama watoto na kuwaambia nini wanatakiwa kufanya katika muda wao wa ziada," Alisema Hodgson mwezi wa pili mwaka huu.
"Siwashauri kwenda mbali wakati wa mapumziko".
0 comments:
Post a Comment