GERARDO
Martino amesema yeye ndiye anatakiwa kulaumiwa kutokana na msimu mbaya wa
Barcelona baada ya kulazimisha sare ya mabao 2-2 nyumbani Camp Nou dhidi ya
Getafe katika mchezo wa La Liga.
Lionel
Messi alikuwa wa kwanza kufunga bao la kuongoza dakika ya 23 kabla ya Angel
Lafita kusawazisha dakika ya 42, lakini Alex Sanchez aliandika bao la pili
dakika ya 67.
Barca
wakiwa na matumaini ya kushinda mechi hiyo, dakika ya 90 ya mchezo, Lafita
alizima ndoto zao baada ya kusawazisha bao la pili na matokeo kubakia 2-2,
lakini Wakalunya hao bado wana matumaini ya kubeba ubingwa.
Martino
baada ya mechi alisema: “Tulifanya makosa yaliyotugharimu. Timu ilikuwa na hamu
ya kushidna”.
“Tulicheza
vizuri na kustahili kushinda. Kiukweli sio msimu mzuri kwetu. Si kwangu tu hata
klabu pia. Umekuwa msimu mgumo mno”.
“Nadhani
anayewajibika kwa hili ni kocha anayeongoza timu. Kimahesabu, tumefanya kila
jitihada kushinda taji.”.
“Tulihitaji
kufanya vitu vingi zaidi, lakini hatutakiwa kukata tamaa mpaka siku ya mwisho”.
Martino
aliendelea kwa kusema kumekuwa na matatizo klabuni ambayo yanatakiwa
kutatuliwa, huku akionesha kutokuwa na wasiwasi juu ya hatima yake.
“Wachezaji
wanajua nini kinaigawa timu na lipi chaguo sahihi”. Alisema.
“Bado
kuna muda wa kueleza hatima yangu. Huwa sioni shida kuwajibika na nadhani
nastahili kubeba lawama. Msimu huu kumekuwa na mapungufu yanayotakiwa
kutatuliwa”.
MATOKEO YA MECHI ZOTE LA LIGA LEO HII HAYA HAPA
SPAIN: Primera Division | |||||||
17:00 | Finished | Barcelona | 2 - 2 | Getafe | |||
19:00 | Finished | Malaga | 0 - 1 | Elche | |||
21:00 | Finished | Osasuna | 0 - 2 | Celta Vigo | |||
23:00 | 15 | Valladolid | 0 - 0 | Espanyol |
RATIBA YA KESHO
Almeria | - | Betis | |||||
18:00 | Levante | - | Atl. Madrid | ||||
20:00 | Sevilla | - | Villarreal | ||||
22:00 | Real Madrid | - | Valencia |
BAADA YA MECHI ZA LEO MSIMAMO WA TIMU 10 ZA JUU UNAKUWA HIVI
Spanish La Liga
Pos | Team | P | W | D | L | GF | GA | GD | Pts |
1 | Atlético de Madrid | 35 | 28 | 4 | 3 | 75 | 22 | 53 | 88 |
2 | Barcelona | 36 | 27 | 4 | 5 | 99 | 32 | 67 | 85 |
3 | Real Madrid | 34 | 26 | 4 | 4 | 98 | 32 | 66 | 82 |
4 | Athletic Club | 36 | 20 | 8 | 8 | 65 | 38 | 27 | 68 |
5 | Sevilla | 35 | 17 | 8 | 10 | 66 | 50 | 16 | 59 |
6 | Real Sociedad | 35 | 16 | 9 | 10 | 59 | 51 | 8 | 57 |
7 | Villarreal | 35 | 15 | 7 | 13 | 54 | 43 | 11 | 52 |
8 | Celta de Vigo | 36 | 13 | 7 | 16 | 46 | 52 | -6 | 46 |
9 | Valencia CF | 35 | 12 | 9 | 14 | 47 | 48 | -1 | 45 |
10 | Rayo Vallecano | 36 | 13 | 4 | 19 | 45 | 74 | -29 | 43 |
0 comments:
Post a Comment