Monday, May 12, 2014



 
CARLO Ancelotti amechizika baada ya Real Madrid kufungwa mabao 2-0 dhidi ya  Celta Vigo katika mchezo wa La Liga na kujitoa rasmi katika mbio za ubingwa,  huku wakisaliwa na mchezo mmoja tu.
Endapo wangeshinda, vijana hao wa Santiago Bernabeu wangepunguza pengo la pointi na kufikia pointi mbili nyuma  ya vinara Atletico na pointi moja mbele ya Barcelona, lakini matokeo ya jumapili yanamaanisha matumaini yamekwisha.
“Rasmi tumekosa La Liga. Ni mashindano ya kwanza msimu huu ambayo hatuwezi kushinda na itakuwa ni uongo kama tukajipa moyo,” Alisema Ancelotti baada ya mechi.
“Tulikosa wachezaji wengi muhimu, kwahiyo haikua rahisi kujiandaa na mechi hii. Tumefungwa mabao mawili mepesi kabisa, lakini tulijaribu kurudi mchezoni  baada ya pale”.
“Tunatakiwa kuangalia ya mbele,  sasa tunajiandaa na mchezo wa mwisho na fainali ya UEFA”.
Real Madrid watakabiliana na Espanyo katika mchezo wa mwisho wa La Liga kabla ya kuumana na Atletico Madrid katika mchezo wa fainali wa UEFA mei 24 mwaka huu mjini Lisbon, Ureno.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video