ARSENAL wamefanikiwa kujihakikishia nafasi ya kucheza
michuano ya UEFA kwa mwaka wa 17 mfululizo baada ya Everton kuchapwa mabao 3-2
na Manchester City na kumhakikishia Aserne Wenger kumaliza ligi si chini ya
nafasi ya nne katika msimamo.
Mabao mawili ya Edin Dzeko na lingine kutoka kwa
Sergio Aguero yametosha kumpatia ushindi Manuel Pellegrini na kupanda kileleni
kwa ligi kuu.
Man City sasa hatima yao ya kubeba ubingwa imebaki
katika mechi zao mbili za mwisho dhidi ya Aston Villa na West Ham ili kuchukua
ubingwa wao wa pili wa ligi kuu katika misimu mitatu.
Asernal walitabiriwa kuchuana na Man City kutafuta
ubingwa msimu huu na waliongoza ligi kwa muda mrefu kabla ya kuanza kupoteza
mechi nyingi na kuwaacha Chelsea na Liverpool wakishindana na Manchester City
mpaka sasa.
Kufungwa na Everton katika uwanja wa Goodison Park
mwezi uliopita kulitaka kutia doa rekodi ya kushiriki UEFA kwa miaka 17
mfululizo, huku Roberto Martinez kwa upande wake toka siku hiyo amefungwa na
Southampton, Crustal Palace na Manchester City.
Sasa Asernal wanajiandaa na michezo yao miwili ya
mwisho dhidi ya West Bromwich Albion na Nowrich ili kujihakikishia nafasi yao
ya nne na kuhamishia akili zao katika fainali ya FA.
Washaki bunduki
hao wa London watakabiliana na Hull City kwenye uwanja wa Wembley mei 17 mwaka
huu, huku wakiwa na matumaini ya kufuta ukame wa kutobeba makombe kwa miaka
tisa sasa.
0 comments:
Post a Comment