WINGA hatari wa Asernal, Theo
Walcott anaamini kushinda taji la FA itakuwa kichocheo cha kushinda mataji
mengi misimu ijayo.
Imepita miaka 9 sasa tangu Arsene
Wenger abebe `ndoo` ambapo kwa mara ya mwisho aliifunga Manchester United kwa
penati na kutwaa kombe la FA mwaka 2005.
Asernal wanayo fursa ya kufuta ukame
huu watakapokutana na Hull City katika mechi ya fainali ya FA mei 17 mwaka huu
na Walcott anaamini wakishinda italeta upepo mpya Emirates.
“Kama tutashinda FA kwa kuzingatia
jinsi tunavyocheza sasa, wachezaji watakuwa na hamu ya makombe zaidi. Walcott
ameiambia Tovuti ya Asernal.
“Nadhani kombe la kwanza ni muhimu-
ukishinda, utashinda mengi zaidi. Nina uhakika na hilo”.
“Itakuwa heshima kwa bosi wetu
kushinda kombe tena”.
“Ametuami kwa miaka yote. Kama hatuchezi
vizuri, siku zote ananyoshewa vidole hata kama ni makosa yetu”.
Asernal walianza kwa kasi msimu huu
na kutabiriwa kushinda taji la ligi kuu nchini England, lakini waliyeyuka mithiri ya
barafu na kuziachia Chelsea, Man City na Liverpool ziendelee kupambana.
Walcott hajapangwa tangu mwezi
januari mwaka huu kutokana na majeruhi, lakini anaamini kurejea kwa Aaron Ramsey, Jack Wilshere na Mesut Ozil kutaweza
kutimiza ndoto zao kuelekea fainali ya FA.
Aliongeza: “Kuwakosa Aaron, Mesut,
na Jack, kocha wetu alisema itakuwa ngumu kuzoeana. Ukiwatoa wachezaji hao
watatu kwenye kikosi, timu itaathirika”.
“Ilikuwa huzuni kwa kila mtu
kuwapoteza wachezaji hawa kwa wakati mmoja, lakini lazima mjitahidi kukaza”.
0 comments:
Post a Comment